Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waroma 12:12 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

12 kwa tumaini, mkifurahi; katika shidda, mkivumilia; katika kusali, mkidumu;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida, na kusali daima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida, na kusali daima.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Tumaini lenu liwaweke daima wenye furaha; muwe na saburi katika shida, na kusali daima.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Kuweni na furaha katika tumaini, katika dhiki kuweni na saburi, dumuni katika maombi.

Tazama sura Nakili




Waroma 12:12
71 Marejeleo ya Msalaba  

Furahini, shangilieni: kwakuwa thawabu yenu nyingi mbinguni; kwa maana ndivyo walivyowatesa manabii waliokuwa kabla yenu.


Lakini msifurahi kwa sababu hii ya kuwa pepo wanawatiini: hali furahini kwa kuwa majina yenu yameandikwa mbinguni.


Kwa subira yenu mtazipata robo zenu.


Nazo penye udongo mwema, hawa ndio ambao kwamba kwa moyo mzuri na mwema hulisikia neno, wakalishika, wakazaa kwa saburi.


Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kuomba, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama wake Yesu, na ndugu zake.


Bassi Petro akalindwa gerezani, sala zikawa zinafanyika kwa juhudi sana na Kanisa mbele za Mungu kwa ajili yake.


Wakawa wakidumu katika fundisho la mitume, na katika ushirika, na katika kuumega mkate, na katika kusali.


na sisi tutadumu katika kumwomba Mungu na kulikhudumia Neno lake.


Bassi Mungu wa tumaini awajazeni furaha yote na amani katika kuamini, mpate kuzidi sana kuwa na tumaini, katika nguvu za Roho Mataktifu.


Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa kutufundisha sisi, illi kwa uvumilivu na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.


wale ambao kwa kustahimili katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutoa kuharibika, nzima wa milele;


Bali tukikitumaini kitu tusichokiona, twakingojea kwa uvumilivu.


Bassi, sasa inabaki imani, tumaini, upendo, hizi tatu; na iliyo kuu katika hizi ni upendo.


Kwa ajili ya kitu hiki nalimsihi Bwaua marra tatu kinitoke.


KHATIMAE, ndugu zangu, furahini katika Bwana. Kuwaandikieni yale yale hakuniudhi mimi, bali kutawafaa niuyi.


Furahini katika Bwana siku zote; marra ya pili nasema, Furahini.


mkiwezeshwa kwa nwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya killa namna na uvumilivu pamoja na furaha;


ambao Mungu alipenda kuwajulisha jinsi ulivyo utajiri wa utukufu wa siri hii katika mataifa, nao ni Kristo ndani yenu, tumaini la utukufu;


Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu, katika maombi yake msimame wakamilifu mkathuhutike sana katika mapenzi yote ya Mungu.


Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani,


wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya amani, na taabu yenu ya upendo, na uvumilivu wenu wa tumaini lililo katika Bwana Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu;


Lakini sisi tulio wa mchana, tuwe na kiasi, tukijivika kifuani imani na upendo, na chepeo yetu iwe tumaini la wokofu.


Hatta sisi wenyewe twajisifu katika makanisa ya Mungu kwa ajili ya uvumilivu wenu, na imani mliyo nayo katika adha zenu zote na mateso mnayoyavumilia;


Bwana awaongozeni mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na uvumilivu wa Kristo.


Bali wewe, mtu wa Mungu, yakimbie hayo, ukafuate haki, utawa, imani, upendo, uvumilivu, upole.


Bali wewe umeyafuata mafundisho yangu, na mwenendo wangu, na makusudi yangu, na imani, na upole, na upendo, na uvumilivu,


tukilitazamia tumaini lenye baraka na mafunuo ya utukufu wa Mungu mkuu, Mwokozi wetu Yesu Kristo;


tukifanyiziwa wema kwa neema yake, tupate kufanywa warithi wa uzima wa milele, kama lilivyo tumaini letu.


Lakini zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu;


Maana mnahitaji uvumilivu, illi mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu muipate abadi.


BASSI na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, tuweke kando killa mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa uvumilivu katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,


bali Kristo, kama mwana, juu ya nyumba yake; ambae nyumba yake ni sisi, kama tukishikamana sana na ujasiri wetu na kujisifu kwetu, kwa kutumaini mpaka mwisho.


Yeye siku hizo za niwili wake alimtolea yeye awezae kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa sababu ya kicho chake;


illi msiwe wavivu, hali wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imaui na uvumilivu.


Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.


Bassi vumilieni, ndugu, hatta kuja kwake Bwana. Mwangalieni mkulima; hungoja mazao ya inchi yaliyo ya thamani, husubiri kwa ajili yake hatta yatakapopata mvua ya kwanza na ya mwisho.


lakini kama mnavyoyashiriki mateso va Kristo furahini; illi na katika ufimuo wa utukufu wake mfurahi kwa shangwe.


Mwisho wa mamho yote umekaribia; bassi, mwe na akili, mkakeshe katika sala:


na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu uvumilivu, na katika uvumilivu wenu utawa,


Mtu akichukua mateka achukuliwa mateka. Mtu akiua kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hivyo ndivyo uvumilivu na imani ya watakatifu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo