Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Waebrania 11:13 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

13 Hawa wote wakafa katika imani, wasizipokee zile ahadi, bali wakiziona tokea mbali na kuzisalimu, na kukiri kwamba walikuwa wageni, na wasafiri juu ya inchi.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Watu hawa wote walikufa wakiwa na imani. Walikufa kabla ya kupokea mambo ambayo Mungu alikuwa ameahidi, lakini kwa mbali waliyaona, wakashangilia, na kukiri wazi kwamba wao walikuwa wageni na wakimbizi duniani.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Watu hawa wote wakafa katika imani bila kuzipokea zile ahadi, lakini waliziona kwa mbali na kuzishangilia. Nao walikubali kwamba walikuwa wageni na wasiokuwa na maskani hapa duniani.

Tazama sura Nakili




Waebrania 11:13
36 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa maana amin, nawaambieni, Manabii wengi na wenye haki walitamani kuyaona mnayoyaona ninyi, wasivaone; na kuyasikia mnayoyasikia, wasiyasikie.


Maneno hayo aliyasema Isaya alipouona utukufu wake, akataja khabari zake.


Ibrahimu baba yemi alishangilia apate kuiona siku yangu; akaona, akafurahi.


akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi.


Kwa maana tuliokolewa kwa kutumaini; lakini kitu kilichotumainiwa kikionekana hakuna kutumaini tena. Kwa maana kile akionacho mtu, ya nini kukitumaini?


tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.


Bassi siku zote tuna moyo mkuu; tena twajua ya kuwa, wakati tuwapo hapa katika mwili, tunakaa mbali ya Bwana.


Bassi tangu sasa ninyi si wapitaji wala wageni, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumba ya Mungu,


Maana wasemao maneno kama hayo waonyesha kwa wazi kwamba wanatafuta inchi yao wenyewe.


Kwa imani Ibrahimu alipojaribiwa, akamtoa Isaak, awe dhabihu; na yeye aliyezipokea ahadi alikuwa akimtoa mwana wake, mzaliwa wake wa pekee;


Kwa imani akatoka Misri, asiogope hasira ya mfalme; maana alistahimili kama amwonae yeye asiyeonekana.


Na watu hawa wote wakiisha kushuhudiwa kwa sababu ya imani yao, hawakuipokea ahadi:


PETRO, mtume wa Yesu Kristo, kwa wateule wa Mtawanyiko, wakaao bali ya wageni katika Ponto, Galatia, Kappadokia, Asia na Bithunia,


Na ikiwa mnamwita Baba yeye ahukumuye killa mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa khofu kafika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni;


Mapenzi, nakusihini kama wapitaji na wasafiri, ziepukeni tamaa za mwili zipiganazo na roho;


Hivi tutafahamu ya kwamba tu wa kweli, na mbele zake tutatuliza mioyo yetu


Tufuate:

Matangazo


Matangazo