Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ufunuo 2:3 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

3 tena ulistahimili na kuwa na uvumilivu, na kwa ajili yangu umejitaabisha wala hukuchoka.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Wewe unayo saburi, umestahimili taabu nyingi kwa ajili ya jina langu, wala hukuvunjika moyo.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.

Tazama sura Nakili




Ufunuo 2:3
49 Marejeleo ya Msalaba  

Wakamtumikisha mtu aliyekuwa akipita, Simon Mkurene, akitoka mashamba, baba wa Iskander na Rufo, auchukue msalaba wake.


Na mfu ye yote asiyechukua msalaba wake na kuja nyuma yangu, hawezi kuwa mwanafunzi wangu.


AKAWAAMBIA na mfano ya kama imewapasa kumwomba Mungu siku zote wala wasikate tamaa,


Kwa subira yenu mtazipata robo zenu.


Simon akajibu, akasema, Bwana, tulisumbuka usiku kucha, tusipate kitu: illakini kwa neno lako nitazishusha nyavu.


Nazo penye udongo mwema, hawa ndio ambao kwamba kwa moyo mzuri na mwema hulisikia neno, wakalishika, wakazaa kwa saburi.


Lakini haya yote watawatenda kwa sababu ya jina langu, kwa kuwa hawamjui aliyenipeleka.


kwa tumaini, mkifurahi; katika shidda, mkivumilia; katika kusali, mkidumu;


Nisalimieni Trufina na Trufosa, wenye ijtihadi katika Kristo.


wale ambao kwa kustahimili katika kutenda mema wanatafuta utukufu na heshima na kutoa kuharibika, nzima wa milele;


Bali tukikitumaini kitu tusichokiona, twakingojea kwa uvumilivu.


hustahimili yote, huamini yote, hutumaini yote, huvumilia yote.


bassi watiini watu kama hawa, na killa mtu afanyae kazi pamoja nao, na kujitaabisha.


wala hatujisifu zaidi ya kadiri yetu, katika kazi za watu wengine; bali tukiwa na tumaini ya kwamba, imani yenu ikuapo, tutakuzwa kwenu kwa kadiri yetu;


Wao wakhudumu wa Kristo? (nanena kiwazimu), mimi zaidi; kwa kazi kuzidi sana; kwa mapigo kupita kiasi; kwa vifungo kuzidi sana; kwa mauti marra nyingi.


KWA sababu hiyo, kwa kuwa tuna khuduma hii, kwa jinsi tulivyorehemiwa, hatulegei;


Kwa hiyo hatuzimii; bali ijapokuwa mtu wetu wa nje unaharibiwa, illakini mtu wetu wa ndani unafanywa npya siku baada ya siku.


Kwa hiyo, tena, ikiwa tupo hapa, au ikiwa hatupo hapa, twajitahidi kumpendeza yeye.


kafika mapigo, katika vifungo, katika fitina, katika kazi, katika kukesha, katika kufunga;


Mchukuliane mizigo mkaitimize hivyo sharia ya Kristo.


Na tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia.


nipate sababu ya kujisifu katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio burre wala sikujitaabisha burre.


Naam, nakutaka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi nae, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.


mkiwezeshwa kwa nwezo wote, kwa kadiri ya nguvu ya utukufu wake, mpate kuwa na saburi ya killa namna na uvumilivu pamoja na furaha;


wala hatuachi kuikumbuka kazi yenu ya amani, na taabu yenu ya upendo, na uvumilivu wenu wa tumaini lililo katika Bwana Yesu Kristo, mbele za Mungu Baba yetu;


Maana, ndugu, mnakumbuka taabu yetu na masumbufu yetu; kwa kuwa mchana na usiku tulifanya kazi tusije tukamlemea mtu wa kwenu, tukawakhubirini bivi Injili ya Mungu.


Lakini, ndugu, tunataka mwajue wale wanaojitaabisha kwa ajili yenu na kuwasimamieni katika Bwana, na kuwaonyeni;


Lakini, ninyi, ndugu, msikate tamaa katika kutenda mema.


Bwana awaongozeni mioyo yenu mkapate pendo la Mungu, na uvumilivu wa Kristo.


wala hatukula chakula kwa mtu ye yote burre, bali kwa taabu na masumbufu, mchana na usiku, tulitenda kazi, illi tusimlemee mtu kwenu;


Kwa maana twajitaabisha na kujitahidi katika jambo hili, kwa sababu twamtumaini Mungu aliye hayi aliye mwokozi wa watu wote, khassa wa hao waaminio.


Wazee watawalao vema wapewe heshima mardufu, khassa wao wajitaabishao kwa kukhutubu na kufundisha.


Maana mnahitaji uvumilivu, illi mkiisha kuyafanya mapenzi ya Mungu muipate abadi.


BASSI na sisi pia, kwa kuwa tunazungukwa na wingu kubwa la mashahidi namna hii, tuweke kando killa mzigo mzito, na dhambi ile ituzingayo kwa upesi; na tupige mbio kwa uvumilivu katika yale mashindano yaliyowekwa mbele yetu,


Bassi na twende kwake nje ya kituo, tukichukua laumu lake.


maana Mungu si dhalimu hatta asahau kazi zenu, na pendo lile mlilolidhihirisha kwa jina lake, kwa kuwa mmewakhudumia watakatifu, na hatta hivi sasa mngali mkiwakhudumia.


illi msiwe wavivu, hali wafuasi wa hao wazirithio ahadi kwa imaui na uvumilivu.


Na hivyo kwa kuvumilia akaipata ile ahadi.


na katika maarifa yenu kiasi, na katika kiasi chenu uvumilivu, na katika uvumilivu wenu utawa,


Mimi Yohana, ndugu yenu na mwenye kushiriki pamoja nanyi katika mateso na ufalme na uvumilivu wa Yesu Kristo, nalikuwa katika kisiwa kiitwacho Patmo, kwa ajili ya Neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu.


Kwa kuwa ulilishika neno la uvumilivu wangu, mimi nami nitakulinda, utoke katika saa ya kujaribiwa iliyo tayari kuujia ulimwengu wote, kuwajaribu wakaao juu ya inchi.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo