Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -




Ufunuo 18:3 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

3 kwa kuwa mataifa yote wamekunywa mvinyo ya ghadhabu ya uasharati wake, na wafalme wa inchi wamezini nae, na matajiri ya inchi wamepata mali kwa nguvu za kiburi chake.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Maana mataifa yote yalileweshwa kwa divai kali ya uzinzi wake, nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye. Nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na anasa zake zisizo na kipimo.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi naye, na wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao, nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”

Tazama sura Nakili




Ufunuo 18:3
17 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini mlitoka kwenda kuona nini? Mtu aliyevikwa mavazi meroro? Fahamuni, watu wenye nguo za umalidadi na kuishi maisha ya anasa wamo katika majumba ya wafalme.


Bali wajane walio vijana nkatae kuwaandika, maana wakiona tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa,


Malaika mwingine akamfuata, akisema, Umeanguka, umeanguka Babeli, mji ule ulio mkubwa, maana ndio uliowanywesha mataifa yote mvinyo ya hasira ya uasharati wake.


ambae wafaime wa inchi walizini nae, nao wakaao katika inchi wakalevywa kwa mvinyo ya uasharati wake.


Wakatupa mavumbi juu ya vichwa vyao, wakalia, wakitoka machozi na kuomboleza, wakisema, Ole, ole wake mji ule ulio mkuu, ambao ndani yake wote wenye merikebu katika bahari walipata mali kwa utajiri wake; kwa kuwa katika saa moja umekuwa ukiwa.


wala nuru ya taa haitamulika ndani yako tena kabisa, wala sauti ya bwana arusi na bibi arusi haitasikiwa ndani yako tena kabisa; maana wafanyi biashara wako walikuwa wakuu wa inchi, kwa kuwa mataifa yote wamedanganywa kwa uchawi wako.


Kwa kadiri aliyojitukuza na kufanya anasa, mpeni maumivu na huzuni kadiri hiyo hiyo. Kwa kuwa alisema moyoni mwake, Nimeketi malkiya, nami si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.


Na wafalme wa inchii waliozini nae na kufanya anasa pamoja nae, watalia na kumwombolezea; wauonapo moshi wa kuumgua kwake,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo