Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Ufunuo 11:3 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

3 Nami nitawarukhusu mashahidi wangu wawili, nao watatoa unabii siku elfu na miateen na sittini, wamevikwa mavazi ya kigunia.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

3 Nami nitawatuma mashahidi wangu wawili ili watoe unabii kwa muda huo wa siku 1,260, wakiwa wamevaa mavazi ya gunia.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

3 Nami nitawatuma mashahidi wangu wawili ili watoe unabii kwa muda huo wa siku 1,260, wakiwa wamevaa mavazi ya gunia.”

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

3 Nami nitawatuma mashahidi wangu wawili ili watoe unabii kwa muda huo wa siku 1,260, wakiwa wamevaa mavazi ya gunia.”

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na sitini, wakiwa wamevaa gunia.”

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

3 Nami nitawapa mashahidi wangu wawili uwezo, nao watoe unabii kwa muda wa siku 1,260, wakiwa wamevaa nguo za gunia.”

Tazama sura Nakili




Ufunuo 11:3
43 Marejeleo ya Msalaba  

Ole wako, Korazin! Ole wako, Bethsaida! Kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu ingalifanyika katika Turo na Sidon, wangalitubu zamani kwa kuvaa gunia na majivu.


La, hakusikia, chukua pamoja nawe tena mtu mmoja au wawili, illi kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu killa neno lithubutike.


Ole wako, Korazin! Ole wako Bethsaida! kwa maana kama miujiza iliyofanyika kwenu, ingalifanyika katika Turo na Sodom, wangalitubu zamani, wakiketi katika nguo za kigunia na majivu.


Nanyi mashahidi wa mambo haya.


Na ninyi pia mnashunudu, kwa kuwa tangu mwanzo mmekuwa pamoja nami.


Yohana akajibu, akasema, Hawezi mtu kupokea neno lo lote isipokuwa amepewa kutoka mbinguni.


Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemi, na katika Yahudi yote, na Samaria, na hatta mwisho wa inchi.


akaonwa siku nyingi nao waliopanda nae kutoka Galilaya hatta Yerusalemi, na hao ndio walio sasa mashahidi wake mbele va watu.


Yesu huyo Mungu alimfufua, na sisi sote tu mashahidi wake.


mkamwua yule Mkuu wa uzima, ambae Mungu amemfufua: na sisi tu mashahidi wake.


Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu, kiisha miujiza, kiisha karama za kuponya wagonjwa, na masaidiano, na kutawala, na aina za lugha.


HII ndio marra ya tatu ya mimi kuja kwenu. Kwa vinywa vya mashahidi wawili au watatu killa neno litathubutishwa.


Na yeye aliwatoa wengine kuwa mitume; na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti, na wengine kuwa wachungaji, na waalimu,


na zitokazo kwa Yesu Kristo, shahidi alive mwaminifu, mzaliwa wa kwanza wa waliokufa, na mkuu wa wafalme wa dunia. Kwake yeye aliyetupeuda na kutuosha dhambi zetu kwa damu yake,


Na behewa iliyo nje ya hekalu uitupe nje wala usiipime, kwa maana mataifa wamepewa hiyo, nao wataukanyaga mji mtakatifu miezi arubaini na miwili.


Hawa wana mamlaka kuzifunga mbingu, illi mvua isinye katika siku za unabii wao. Na wana mamlaka juu ya maji kuyagenza kuwa damu, na kuipiga inchi kwa killa pigo, killa watakapo.


Yule mwanamke akakimbilia nyikani ambapo ana mahali palipotengenezwa na Mungu, illi wamlishe huku siku elfu na miateen na sittini.


Akapewa kinywa kunena maneno makuu, ya ukafiri. Akapewa uwezo kufanya kazi yake miezi arubaini na miwili.


Nikaanguka mbele ya miguu yake, nimsujudie, akaniambia, Angalia, usifanye hivi: mimi mjoli wako na mmoja wa ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Msujudu Mungu: kwa maana ushuhuda wa Yesu ni roho ya unabii.


Nikaona viti vya enzi, wakaketi juu yake, wakapewa hukumu: nikaona roho zao waliokatwa kichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia nyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea alama yake katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; wakawa hayi, wakamiliki pamoja na Kristo miaka elfu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo