Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Tito 2:11 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

11 Maana neema ya Mungu iwaokoayo wana Adamu wote imeonekana;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

11 Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

11 Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

11 Maana neema ya Mungu imedhihirishwa kwa ajili ya wokovu wa watu wote.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

11 Kwa maana neema ya Mungu ambayo inawaokoa wanadamu wote imefunuliwa.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

11 Kwa maana neema ya Mungu ambayo inawaokoa wanadamu wote imefunuliwa.

Tazama sura Nakili




Tito 2:11
50 Marejeleo ya Msalaba  

Bassi, enendeni, kawafanyeni mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba, na Mwana, na Roho Mtakatifu;


Akawaambia, Enendem nlimwenguni mwote, mkaikhubiri injili kwa killa kiumbe.


na mataifa yote wakhubiriwe kwa jina lake toba na ondoleo la dhambi, kuanzia Yerusalemi.


Na wote wenye mwili watanona wokofu wa Mungu.


Nae Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu, tukautazama utukufu wake, utukufu kama wa Mwana pekee akitoka kwa Baba, amejaa neema na kweli.


Kulikuwako nuru halisi, imtiayo nuru killa mtu ajae katika ulimwengu.


Nae, alipokwisha kufika na kuiona neema ya Mungu akafurahi, akawasihi wote waambatane na Bwana kwa kusudi la moyo.


Sunagogi lilipofumukana, Wayahudi wengi na waongofu watawa wakashikamana na Paolo na Barnaba; nao, wakisema nao, wakawatia moyo kudumu katika neema ya Mungu.


Kwa sababu ndivyo tulivyoamriwa na Bwana, Nimekuweka uwe nuru ya mataifa, Upate kuwa wokofu hatta mwisho wa dunia:


Bassi zamani zile za ujinga Mungu alijifanya kama hauoni; bali sasa anawakhuhiri watu wote wa killa mahali watubu.


Lakini siyahesabu maisha yaugu kuwa kitu cha thamani kwangu kama kuumaliza mwendo wangu na khuduma ile niliyopokea kwa Bwana Yesu, kuishuhudia Injili ya neema ya Mungu.


Lakini nasema, Wao hawakusikia? Naam, wamesikia, Sauti yao imetoka ikaenea katika inchi yote, Na maneno yao hatta miisho ya ulimwengu.


Lakini kipawa kile hakikuwa kama lile kosa; kwa maana ikiwa kwa kuanguka kwake yule mmoja wengi walikufa, zaidi sana neema ya Mungu, na kipawa kilicho katika neema ya mtu mmoja Yesu Kristo kimezidi kwa ajili ya wale wengi.


kwa yeye tumepata kwa njia ya imani kuifikia neema hii ambayo tunasimama ndani yake; na twafurahi katika tumaini la utukufu wa Mungu.


NASI tukitenda kazi pamoja nae tunakusihini msiipokee neema ya Mungu burre,


Siibatili neema ya Munga. Maana, ikiwa haki hupatikana kwa sharia, bassi, Kristo alikufa burre.


hatta wakati ule tulipokuwa wafu kwa sababu ya makosa yetu, alituhuisha pamoja na Kristo (mmeokolewa kwa neema);


Maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; na hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu:


mkidumu tu katika imani, mmewekwa juu ya misingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia khabari zake, iliyokhubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paolo nalikuwa mkhudumu wake.


iliyofika kwenu, kama ilivyo katika ulimwengu wote, ikizaa matunda na kukua, kama na inavyokua kwenu, tangu siku mliposikia nikaifahamu sana neema ya Mungu katika kweli;


Na Bwana wetu Yesu Kristo, na Mungu Baba yetu aliyetupenda akatupa faraja ya milele na tumaini jema, katika neema,


na neema ya Bwana wetu ilizidi sana pamoja na imani na pendo lililo katika Kristo Yesu.


atakae watu wote waokolewe wakapate kujua sana yaliyo kweli.


na sasa inadhihirishwa kwa kufunuliwa kwake Mwokozi wetu Yesu Kristo, aliyebatili mauti na kuufunua uzima ua kutoa kuharibika, kwa ile Injili,


Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu, illi kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu, mataifa wrote wakasikie; nikaokolewa katika kanwa la simba.


mkiangalia sana mtu asiipungukie neema ya Mungu; shina la uchungu lisije likachipuka na kuwasumbua watu wengi, wakatiwe najis kwa hilo.


illa twamwona yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, illi kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya killa mtu.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo