Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




Matendo 13:32 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

32 Na sisi tunawakhubirieni ahadi ile waliyopewa baba zetu, ya kwamba Mungu ametutimizia sisi watoto wao ahadi hiyo, kwa kumfufua Yesu:

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

32 Nasi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: Jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

32 Nasi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: Jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu,

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

32 Nasi tumekuja hapa kuwaleteeni Habari Njema: jambo lile Mungu alilowaahidia babu zetu,

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

32 “Nasi tunawaletea Habari Njema: kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

32 “Nasi tunawaletea habari njema, kwamba yale Mungu aliyowaahidi baba zetu

Tazama sura Nakili




Matendo 13:32
40 Marejeleo ya Msalaba  

Malaika akamjibu, akamwambia, Mimi ni Gabrieli nisimamae mbele ya Mungu: nami nalitumwa niseme nawe, na kukupasha khabari hizi njema.


Malaika akawaambia, Msifanye khofu; kwa maana nawaletea ninyi khabari njema za furaha kuu, itakayokuwa kwa watu wote:


Neno lile alilowapelekea wana wa Israeli, akikhubiri amani kwa Yesu Kristo (ndiye Bwana wa wote),


Katika uzao wake mtu huyo Mungu amewaletea Israeli Mwokozi, yaani Yesu, kama alivyoahidi,


Bassi, ibainike kwenu, ndugu, ya kuwa kwa huyu mnakhubiriwa ondoleo la dhambi;


Sisi nasi tu wana Adamu hali moja na ninyi; twawakhubiri khabari njema mgenke na kuyaacha mambo haya ya ubatili na kumwelekea Mungu aliye hayi, aliyeumba mbingu na inchi na bahari na vitu vyotc vilivyomo:


Na sasa ninasimama hapa nihukumiwe kwa ajili ya tumaini la ahadi waliyopewa baba zetu na Mungu,


Tubuni bassi, mrejee, illi dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuhurudishwa kwa kuwako kwake Bwana:


Na killa siku ndani ya hekalu na nyumbani mwao, hawakuacha kufundisha na kukhubiri khabari njema za Yesu kwamba ni Kristo.


ambayo Mungu amekwisha kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika maandiko matakatifu,


Tena wakhubirije, wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, Ni mizuri namna gani miguu yao wakhubirio khabari ya mema.


Kwa maana ahadi ile ya kwamba atakuwa mrithi ulimwengu alipewa Ibrahimu na uzao wake, si kwa sharia bali kwa wema aliopata kwa imani.


ambao ni Waisraeli, wenye kufanywa wana, wenye utukufu na maagano, wenye kupewa torati na ibada ya Mungu na ahadi zake; ambao mababu ni wao,


Tufuate:

Matangazo


Matangazo