Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




1 Wakorintho 4:12 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

12 tena twataabika tukifanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa twabariki, tukiudhiwa twavumilia;

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

12 Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

12 Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

12 Tena twataabika na kufanya kazi kwa mikono yetu wenyewe. Tukitukanwa, tunawatakia baraka; tukidhulumiwa, tunavumilia;

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

12 Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki; tunapoteswa, tunastahimili;

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

12 Tunafanya kazi kwa bidii kwa mikono yetu wenyewe. Tunapolaaniwa, tunabariki, tunapoteswa, tunastahimili,

Tazama sura Nakili




1 Wakorintho 4:12
23 Marejeleo ya Msalaba  

M kheri ninyi watakapowatukana na kuwatesa na kuwanenea killa neno baya kwa uwongo, kwa ajili yangu.


bali mimi nawaambieni, Wapendeni adui zenu, wabarikini wanaowalaani, watendeni mema wanaowachukia, waombeeni wanaowatendea ukorofi, na kuwatesa;


Yesu akasema, Baba, uwasamehe, kwa maana hawajui watendalo. Wakagawanya nguo zake, wakipiga kura.


wabarikini wao wawalaanio ninyi, waombeeni wao watendao ninyi jeuri.


Likumbukeni lile neno nililowaambieni, Mtumwa si mkubwa kuliko Bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi nanyi: ikiwa walilishika neno langu, watalishika na lenu.


Akafika kwao; na kwa kuwa kazi yake na kazi yao ni moja, akakaa kwao, akafanya kazi yake, kwa maana walikuwa mafundi wa kufanyiza khema.


Ninyi wenyewe mnajua ya kuwa mikono hii imetumika kwa mahitaji yangu na yao walio pamoja nami.


Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala.


Wabarikini wanaowafukuzeni; barikini, wala msilaani.


Bassi adui yako akiwa na njaa, mlishe; akiwa na kiu, mnyweshe; maana ufanyapo hivi, utampalia makaa ya moto kichwani pake.


Ni nani atakaetutenga na upendo wa Kristo, Je! ni shidda, au dhiiki, au adha, au njaa, au uchi, au khatari, au upanga?


Au je! ni mimi peke yangu na Barnaba tusio na uwezo kutokufanya kazi?


Naliwanyangʼanya makanisa mengine mali yao, nikitwaa posho langu niwakhudumie ninyi.


Mwibaji asiibe tena; bali afadhali afanye juhudi, akitenda kazi iliyo njema kwa mikono yake mwenyewe, apafe kuwa na kitu cha kumgawia mhitaji.


Maana, ndugu, mnakumbuka taabu yetu na masumbufu yetu; kwa kuwa mchana na usiku tulifanya kazi tusije tukamlemea mtu wa kwenu, tukawakhubirini bivi Injili ya Mungu.


wala hatukula chakula kwa mtu ye yote burre, bali kwa taabu na masumbufu, mchana na usiku, tulitenda kazi, illi tusimlemee mtu kwenu;


Kwa maana twajitaabisha na kujitahidi katika jambo hili, kwa sababu twamtumaini Mungu aliye hayi aliye mwokozi wa watu wote, khassa wa hao waaminio.


yeye alipotukanwa, hakurudisha matukano; alipoteswa hakuogofya; bali alijikabidhi kwake yeye ahukumuye kwa haki;


Lakini mjapoteswa kwa sababu ya haki, in kheri; msiogope kutisha kwao, wala msifadhaike;


watu wasiolipa baya badala ya baya, au laumu badala ya laumu; bali wabarikio; kwa sababu ndiyo mlioitiwa illi mrithi baraka.


Bassi wao wateswao apendavyo Mungu na wamwekee roho zao kama amana, katika kutenda mema, kama kwa Muumba mwaminifu.


Lakini Mikael, malaika mkuu, aliposhindana na Shetani, na kuhujiana nae kwa ajili ya mwili wa Musa, hakuthubutu kumshitaki kwa kumlaumu, bali alisema, Bwana akukemee.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo