Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




1 Wakorintho 16:13 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

13 Kesheni, simameni imara katika Imani, mwe waume, mwe hodari.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

13 Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

13 Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

13 Kesheni, simameni imara katika imani, muwe hodari na wenye nguvu.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

13 Kesheni; simameni imara katika imani; kuweni mashujaa na hodari.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

13 Kesheni, simameni imara katika imani, fanyeni kiume, kuweni mashujaa kuweni hodari.

Tazama sura Nakili




1 Wakorintho 16:13
53 Marejeleo ya Msalaba  

Bassi kesheni, maana hamwijui siku wala saa ajapo Mwana wa Adamu.


Kesheni, kaombeni, msije mkaingia majaribuni: Roho ina nia njema, bali mwili ni dhaifu.


Kwa hiyo kesheni killa wakati, mkiomba mpate kuhesabiwa kuwa mmestahili kuponea haya yote yatakayokuwa, na kusimama mahali penu mbele ya Mwana wa Adamu.


Ndugu, msiwe watoto katika akili zenu; illakini katika uovu mwe watoto wachanga, bali katika akili zenu mwe watu wazima.


Bassi, ndugu wapendwa, mwe imara, msiotikisika, mkizidi sana kutenda kazi ya Bwana siku zote, kwa kuwa taabu yenu siyo burre katika Bwana.


Si kwamba tunatawala imani yenu; hali tu wasaidizi wa furaha yenu; maana mnasimama kwa imani.


KRISTO alitufanya huru kwa uhuru; bassi, simameni, msinaswe tena kwa kifungo cha utumwa.


awajalieni, kwa kadiri ya utajiri wa utukufu wake, kufanywa imara kwa nguvu, kwa kazi ya Roho yake, katika mtu wa ndani;


Ndugu zangu, mwe hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.


Lakini mwenendo wenu uwe kama inavyoipasa Injili ya Kristo, illi, nikija na kuwaona ninyi, au nisipokuwapo, niyasikie mambo yenu, kama mnasimama imara katika roho moja, kwa moyo mmoja mkiishindania imani ya Injili;


BASSI, ndugu zangu, wapendwa wangu, ninaowaonea shauku, furaha yangu, na taji yangu, simameni imara katika Bwana, wapenzi wangu.


Nayaweza mambo yote katika yeye anitiae nguvu.


mkidumu tu katika imani, mmewekwa juu ya misingi, mkawa imara; msipogeuzwa na kuliacha tumaini la Injili mliyosikia khabari zake, iliyokhubiriwa katika viumbe vyote vilivyo chini ya mbingu; ambayo mimi Paolo nalikuwa mkhudumu wake.


Epafra, aliye mtu wa kwenu, mtumwa wa Yesu Kristo, awasalimu, akifanya bidii siku zote kwa ajili yenu, katika maombi yake msimame wakamilifu mkathuhutike sana katika mapenzi yote ya Mungu.


Dumuni sana katika kuomba, mkikesha katika kuomba huku na shukrani,


Kwa kuwa sasa twaishi, ikiwa ninyi mnasimama imara katika Bwana.


Bassi tusilale kama wengine, bali tukeshe, na kuwa na kiasi.


Bassi, ndugu, simameni imara, mkayashike mapokeo mliyofundishwa, ikiwa kwa maneno, au kwa waraka wetu.


Fanya vita vile vizuri vya imani, shika uzima wa milele ulioitiwa, ukayaungama maungamo mazuri mbele ya mashahidi wengi.


BASSI wewe, mwanangu, uwe hodari katika neema iliyo katika Kristo Yesu.


Bali wewe erevuka katika yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mwinjilisti, timiliza khuduma yako.


Nimevifanya vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda;


Mwisho wa mamho yote umekaribia; bassi, mwe na akili, mkakeshe katika sala:


Erevukeni, kesheni; kwa kuwa mshitaki wenu Shetani, kama simba angurumae, huzungukazunguka, akitafuta mtu amle;


Tazama, naja kama mwizi. Yu kheri akeshae, na kuyatunza mavazi yake, asiende uchi wakaone aibu yake.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo