Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -




1 Timotheo 5:17 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

17 Wazee watawalao vema wapewe heshima mardufu, khassa wao wajitaabishao kwa kukhutubu na kufundisha.

Tazama sura Nakili


Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

17 Viongozi wa kanisa wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema - BHND

17 Viongozi wa kanisa wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha.

Tazama sura Nakili

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

17 Viongozi wa kanisa wanaowaongoza watu vizuri wanastahili kupata riziki maradufu, hasa wale wanaofanya bidii katika kuhubiri na kufundisha.

Tazama sura Nakili

Neno: Bibilia Takatifu

17 Wazee wa kundi la waumini wanaoongoza shughuli za kundi hilo vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha.

Tazama sura Nakili

Neno: Maandiko Matakatifu

17 Wazee wa kundi la waumini wanaoongoza shughuli za kundi hilo vizuri wanastahili heshima mara mbili, hasa wale ambao kazi yao ni kuhubiri na kufundisha.

Tazama sura Nakili




1 Timotheo 5:17
41 Marejeleo ya Msalaba  

Angalieni, nimetangulia kuwaambieni.


Kaeni katika nyumba hiyo hiyo, mkila na kunywa vya kwao; kwa maana mtenda kazi astahili kupewa ijara yake.


Bwana akasema, Nani, bassi, aliye wakili mwaminifu niwenye busara, ambae Bwana wake atamweka juu ya ntumishi wake wote, awape watu posho lao kwa saa yake?


Mimi naliwatuma myavune msiyoyataabikia; wengine walitaabika, nanyi mmeingia katika taabu yao.


Wakafanya hivyo, wakawapelekea wazee kwa mikono ya Barnaha na Saul.


Nimewapeni mfano katika mambo yote ya kuwa kwa kushika kazi hivi imewapaseni kuwasaidia wasio na nguvu, na kuyakumbuka maneno ya Bwana Yesu, jinsi alivyosema mwenyewe, Ni kheri kutoa kuliko kupokea.


Na tulipoondoka wakatupakilia vitu vile tulivyokuwa na haja navyo.


mwenye kuonya, katika kuonya kwake; mwenye kukarimu, kwa moyo mweupe; mwenye kusimamia, kwa bidii; mwenye kurehemu, kwa furaha.


Naam, imewapendeza, tena wanawiwa nao. Kwa maana ikiwa mataifa wameyashiriki mambo yao ya roho, imewabidi kuwakhudumu kwa mambo yao ya mwili.


Nisalimieni Trufina na Trufosa, wenye ijtihadi katika Kristo.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa nilivyo; na neema yake iliyo kwangu ilikuwa si burre, bali nalizidi sana kushika kazi kupita wao wote; wala si mimi, bali neema ya Mungu pamoja nami.


bassi watiini watu kama hawa, na killa mtu afanyae kazi pamoja nao, na kujitaabisha.


Maana ninyi mwafanya kazi pamoja na Mungu: ninyi m shamba la Mungu, m jengo la Mungu.


NASI tukitenda kazi pamoja nae tunakusihini msiipokee neema ya Mungu burre,


Mwanafunzi na amshirikishe mkufunzi wake katika mema yote.


nipate sababu ya kujisifu katika siku ya Kristo, ya kuwa sikupiga mbio burre wala sikujitaabisha burre.


Mpokeeni, bassi, katika Bwana, kwa furaha yote, mkawahesabu watu kama huyu kuwa watu wa kuheshimiwa.


Naam, nakutaka na wewe pia, mjoli wa kweli, uwasaidie wanawake hao; kwa maana waliishindania Injili pamoja nami, na Klementi nae, na wale wengine waliotenda kazi pamoja nami, ambao majina yao yamo katika kitabu cha uzima.


(mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje kanisa la Mungu?)


Kwa maana twajitaabisha na kujitahidi katika jambo hili, kwa sababu twamtumaini Mungu aliye hayi aliye mwokozi wa watu wote, khassa wa hao waaminio.


Usiache kuitumia ile karama iliyo udani yako uliyopewa wewe kwa unabii, na kwa kuwekewa mikono ya wazee.


Jitunze nafsi yako, na yale mafundisho. Ukadumu katika hayo; maana kwa kufanya hivi utajiokoa nafsi yako nao wakusikiao.


Ukiwakumhusha ndugu hayo, utakuwa mkhudumu mwema wa Yesu Kristo, na mzoevu wa maneno ya imani, na ya mafundisho yale mazuri uliyoyafuata.


Usikubali mashitaka juu ya mzee, illa kwa vinywa vyao mashahidi wawili au watatu.


Waheshimu wajane walio wajane kweli kweli.


Yampasa mkulima mwenye taabu ya kazi kuwa wa kwanza wa kuyashiriki matunda.


likhubiri neno, fanya bidii, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, kaonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.


Watiini walio na mamlaka juu yenu, na kujinyenyekea kwao; maana wao wanakesha kwa ajili ya roho zenu, kama watu watakaotoa hesabu, illi wafanye hivyo kwa furaha wala si kwa kuugua; maana isingewafaa ninyi.


Wasalimuni wote walio na mamlaka juu yenu, na watakatifu wote; walio wa Italia wanakusalimuni.


Wakumbukeni wale waliokuwa na mamlaka juu yenu, waliowaambia neno la Mungu; tena, kwa kuuchunguza sana mwisho wa maisha zao, iigeni imani yao.


Tufuate:

Matangazo


Matangazo