Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 82 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Ombi la kupata haki Zaburi ya Asafu.

1 Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu.

2 Hadi lini mtahukumu kwa dhuluma, Na kuzikubali nyuso za wabaya?

3 Mfanyieni hukumu maskini na yatima; Mtendeeni haki aliyeonewa, na fukara;

4 Mwokoeni maskini na mhitaji; Mwopoeni mikononi mwa wadhalimu.

5 Hawajui wala hawafahamu, hutembea gizani; Misingi yote ya nchi imetikisika.

6 Mimi nimesema, Ndinyi miungu, Na wana wa Aliye Juu, enyi nyote.

7 Lakini mtakufa kama wanadamu, Mtaanguka kama mmoja wa wakuu.

8 Ee Mungu, usimame, uihukumu nchi, Maana mataifa yote ni yako.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo