Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -

Zaburi 6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Sala ya kuponywa ugonjwa hatari Kwa mwimbishaji: kwa ala za muziki zenye nyuzi; kulingana na mtindo wa Sheminithi. Zaburi ya Daudi.

1 BWANA, usinikemee kwa hasira yako, Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.

2 BWANA, unifadhili, maana ninanyauka; BWANA, uniponye, mifupa yangu imefadhaika.

3 Na nafsi yangu imefadhaika sana; Na Wewe, BWANA, hadi lini?

4 BWANA urudi, uniopoe nafsi yangu, Uniokoe kwa ajili ya fadhili zako.

5 Maana mautini hapana kumbukumbu lako; Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?

6 Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakibubujikia kitanda changu; Nililowesha godoro langu kwa machozi yangu.

7 Macho yangu yameharibika kwa masumbufu, Na kuchakaa kwa sababu yao wanaoniudhi.

8 Ondokeni kwangu, ninyi nyote mtendao uovu; Kwa kuwa BWANA ameisikia sauti ya kilio changu.

9 BWANA ameisikia dua yangu; BWANA atayatakabali maombi yangu.

10 Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, Watarudi nyuma, kwa ghafla wataaibika.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo