Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Mwamini Mungu katika dhiki Zaburi ya Daudi alipomkimbia mwanawe, Absalomu.

1 BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi, Ni wengi wanaonishambulia,

2 Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu, Hana wokovu huyu kwa Mungu.

3 Lakini Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.

4 Kwa sauti yangu namwita BWANA Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.

5 Nilijilaza na kulala usingizi, kisha ninaamka tena, Kwa kuwa BWANA ananitegemeza.

6 Sitayaogopa maelfu na maelfu ya watu, Waliojipanga Juu yangu pande zote.

7 BWANA, uinuke, Mungu wangu, uniokoe, Maana umewapiga taya adui zangu wote; Umewavunja meno wasio haki.

8 Wokovu ni wa BWANA; Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo