Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 20 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Sala ya ushindi Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.

2 Akutumie msaada toka patakatifu pake, Na kukutegemeza toka Sayuni.

3 Azikumbuke sadaka zako zote, Na kuzitakabali dhabihu zako.

4 Akujalie kwa kadiri ya haja ya moyo wako, Na kukutimizia mipango yako yote.

5 Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. BWANA akutimizie matakwa yako yote.

6 Sasa najua kuwa BWANA amwokoa masihi wake; Atamjibu toka mbingu zake takatifu, Kwa matendo makuu ya wokovu Ya mkono wake wa kulia.

7 Hawa wanataja magari na hawa farasi, Lakini sisi tutalitaja jina la BWANA, Mungu wetu.

8 Wao wameinama na kuanguka, Bali sisi tumeinuka na kusimama.

9 BWANA, umwokoe mfalme, Utuitikie siku tuitayo.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo