Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 149 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Sifa kwa wema wa Mungu kwa Israeli

1 Haleluya. Mwimbieni BWANA wimbo mpya, Sifa zake katika kusanyiko la watauwa.

2 Israeli na amfurahie Yeye aliyemwumba, Wana wa Sayuni na wamshangilie mfalme wao.

3 Na walisifu jina lake kwa kucheza, Kwa sauti tamu ya matari na kinubi.

4 Kwa kuwa BWANA awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.

5 Watauwa na waushangilie utukufu, Waimbe kwa sauti kuu vitandani mwao.

6 Sifa kuu za Mungu na ziwe vinywani mwao, Na upanga mkali kuwili mikononi mwao.

7 Ili kufanya kisasi juu ya mataifa, Na adhabu juu ya makabila ya watu.

8 Wawafunge wafalme wao kwa minyororo, Na wakuu wao kwa pingu za chuma.

9 Kuwafanyia hukumu iliyoandikwa; Hiyo ndiyo heshima ya watauwa wake wote. Haleluya.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo