Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 142 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Sala ya ukombozi kutoka kwa watesi Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Ombi.

1 Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA, Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.

2 Nitafunua mbele zake malalamiko yangu, Shida yangu nitaitangaza mbele zake.

3 Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu; Katika njia niendayo wamenifichia mtego.

4 Utazame mkono wangu wa kulia ukaone, Kwa maana sina mtu anijuaye. Makimbilio yamenipotea, Hakuna wa kunitunza roho.

5 BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu, Fungu langu katika nchi ya walio hai.

6 Ukisikilize kilio changu, Kwa maana nimedhilika sana. Uniponye kutoka kwa wanaonifuatia, Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.

7 Uitoe nafsi yangu kifungoni. Nipate kulishukuru jina lako. Wenye haki watanizunguka, Kwa kuwa Wewe unanikirimu.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo