Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Zaburi 13 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Sala ya ukombozi kutoka kwa adui Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.

1 Ee BWANA, utanisahau hadi lini, hata milele? Hadi lini utanificha uso wako?

2 Nitakuwa na wasiwasi rohoni mwangu hadi lini, Nikihuzunika moyoni mchana kutwa? Adui yangu atatukuka juu yangu hadi lini?

3 Ee BWANA, Mungu wangu, uangalie, uniitikie; Uyatie nuru macho yangu, Nisije nikalala usingizi wa mauti.

4 Adui yangu asije akasema, Nimemshinda; Watesi wangu wasifurahi ninapoondoshwa.

5 Lakini mimi nimezitumainia fadhili zako; Moyo wangu na uufurahie wokovu wako.

6 Naam, nitamwimbia BWANA, Kwa kuwa amenitendea kwa ukarimu.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo