Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni
- Matangazo -

Yobu 25 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC


Bildadi anena: Mtu awezaje kuwa mwenye haki mbele za Mungu

1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,

2 Enzi na hofu zi pamoja na Mungu; Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.

3 Je! Majeshi yake yahesabika? Ni nani asiyetokewa na mwanga wake?

4 Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu? Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?

5 Tazama, hata mwezi hauangazi, Wala nyota si safi machoni pake;

6 Seuze mtu, aliye mdudu! Na mwanadamu, ambaye ni buu!

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.

Bible Society of Kenya
Tufuate:



Matangazo