Biblia Todo Logo
Biblia ya mtandaoni

- Matangazo -

Marko 12 - New Testament in Swahili (Zanzibar) Revised Edition 1921

1 AKAANZA kusema nao kwa mifano. Mtu alipanda mizabibu, akazungusha nzio, akachimbia shimo lake shinikizo, akajenga mnara, akapangisha wakulima, akasafiri.

2 Hatta kwa wakati wake akatuma mtumwa kwa wale wakulima, illi apokee kwa wakulima baadhi ya matunda ya mizabibu.

3 Wakamtwaa, wakampiga, wakamtoa nje, hana kitu. Akatuma tena kwao mtumwa mwingine.

4 Na huyo wakampiga mawe, wakamtia jeraha ya kichwa, wakamtoa ametiwa aibu.

5 Akamtuma mwingine, huyo wakamwua; na wengine wengi, wakiwapiga hawa, na wakiwana hawa.

6 Bassi alikuwa na mwana mmoja bado, mpendwa wake; huyu nae akamtuma kwao wa mwisho, akinena, Watamjali mwana wangu.

7 Wale wakulima wakasemezana, Huyu ni mrithi; haya, na tumwue, na urithi utakuwa wetu.

8 Wakamkamata, wakamwua, wakamtupa nje ya shamba la mizabibu.

9 Bassi atafanyani yule Bwana wa mizabibu? Atakuja na kuwaangamiza wale wakulima, na lile shamba la mizabibu atawapa watu wengine.

10 Hatta andiko hili hamjalisoma? Jiwe walilokataa waashi Hili limekuwa jiwe kuu la pembeni.

11 Neno hili limetoka kwa Bwana Nalo ni ajabu machoni petu.

12 Wakatafuta kumkamata, wakaogopa makutano; maana walitambua ya kwamba ule mfano amewanena wao. Wakamwacha wakaenda zao.

13 Wakatuma kwake baadhi ya Mafarisayo na Maherodiano, illi wamnase kwa maneno.

14 Hatta walipofika wakamwambia, Mwalimu, twajua ya kuwa wewe u mtu wa kweli, wala hujali cheo cha mtu; kwa maana hutazami sura za watu: lakini katika kweli waifundisha njia ya Mungu. Je! ni halali kumpa Kaisari kodi au sivyo? Tumpe, tusimpe?

15 Nae, akijua unafiki wao, akawaambia, Mbona mmenijaribu? nileteeni dinari niione. Wakaleta.

16 Akawaambia, Ya nani sanamu hii na anwani hii?

17 Wakamwambia, Ya Kaisari. Yesu akajibu, akawaambia, Mpeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu. Wakamtaajahia sana.

18 Na Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hapana kiyama, wakamwendea,

19 wakamwuliza wakinena, Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mke wake wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mke wake akampatie ndugu yake mzao.

20 Bassi palikuwa na ndugu saba; wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.

21 Wa pili nae akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao.

22 Hatta na wa tatu kadhalika; wukamtwaa wote saba wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa nae.

23 Bassi, katika kiyama watakapofufuka atakuwa mke wa nani katika hawa? Maana wote saba walikuwa nae.

24 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hamjidanganyi kwa sababu hii, kwa kuwa bamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?

25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaozwi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni.

26 Na katika khabari ya wafu ya kwamba wafufuka, hamjasoma katika Kitabu cha Musa, mwenye Kijiti, jinsi Mungu alivyomwambia, akinena, Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, na Mungu wa Isaak, na Mungu wa Yakobo?

27 Yeye si Mungu wa wafu, bali wa wahayi. Kwa hiyo mwajidanganya sana.

28 Mmojawapo wa waandishi akafika, amewasikia wakisemezana nae, akatambua ya kuwa amewajibu vema, akamwuliza, Katika amri zote ipi iliyo ya kwanza?

29 Yesu akamjibu, Katika amri zote ya kwanza ndiyo hii, Sikia, Israeli, Bwana Mungu wetu ni Bwana mmoja;

30 nawe mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote, na kwa nguvu zako zote. Amri ya kwanza ndiyo hii.

31 Na ya pili yafanana na bayo, ndiyo hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Hapana nyingine iliyo kuu kuliko hizi.

32 Yule mwandishi akamwambia, Hakika, mwalimu, umesema vema ya kwamba Mungu ni mmoja, wala hapana mwingine illa yeye:

33 na kumpenda kwa moyo wote, na kwa ufahamu wote, na kwa roho yote, na kwa nguvu zote, na kumpenda jirani kama nafsi yako, kwafaa kuliko kafara zote na dhabihu zote.

34 Yesu, alipoona kwamba amejibu kwa busara, akamwambia, Wewe huwi mbali na ufalme wa Mungu. Wala hakuthubutu mtu kumsaili neno tena tokea hapo.

35 Hatta Yesu alipokuwa akifundisha katika hekalu, akajibu, akanena, Kwa maana gani waandishi hunena ya kwamba Kristo yu Mwana wa Daud?

36 Kwa sababu Daud mwenyewe alisema, kwa uwezo wa Roho Mtakatifu, Bwana alimwambia Bwana wangu, Keti mkono wangu wa kuume Hatta niwafanyapo adui zako kuwa chini ya miguu yako.

37 Daud mwenyewe amwita Bwana: bassi amekuwaje mwana wake? Na ule mkutano mkubwa walikuwa wakimsikiliza kwa furaha.

38 Akawaambia katika mafundisho yake, Jibadharini na waandishi, wapendao kutembea wamevaa mavazi marefu, na kusalimiwa masokoni,

39 na kukaa mbele katika sunagogi, na mahali pa mbele katika karamu:

40 wanakula nyumba za wajane, na kwa unafiki husali sala ndefu: hawa watapokea hukumu iliyo kubwa.

41 Yesu akaketi kuielekea sanduku ya hazina, akatazama jinsi makutano watiavyo fedha katika sanduku. Matajiri wengi wakatia vingi.

42 Akaja mwanamke mmoja, mjane, maskini, akatia sarafu mbili za shaba, kiasi cha nussu pesa.

43 Akawaita wanafunzi wake, akawaambia, Amin, nawaambieni, Huyu mjane maskini ametia vingi kuliko wote wanaotia katika sanduku ya hazina:

44 maana hawa wote walitia baadhi ya mali iliyowazidi: bali huyu katika mahitaji yake ametia vyote alivyokuwa navyo, ndio maisha yake yote pia.

Swahili New Testament © Bible Society of Tanzania, 1921.

Bible Society of Tanzania
Tufuate:



Matangazo