Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 4:1 - Swahili Revised Union Version

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Uliniokoa nilipokuwa katika shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia sala yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia sala yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ee Mungu mtetezi wa haki yangu, unijibu niombapo. Nilipokuwa katika shida, wewe ulinisaidia; unionee huruma na kusikia sala yangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nijibu nikuitapo, Ee Mungu wangu mwenye haki! Nipumzishe katika shida zangu; nirehemu, usikie ombi langu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee Mungu wa haki yangu, uniitikie niitapo; Uliniokoa nilipokuwa katika shida; Unifadhili na kuisikia sala yangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 4:1
35 Marejeleo ya Msalaba  

Naam, yeye angekuongoza utoke katika msiba Hata mahali penye nafasi, ambapo hapana kizuizi; Na kilichowekwa mezani pako kingejaa mafuta.


Kwa kuwa BWANA ni mwenye haki, Apenda matendo ya haki, Wanyofu wa moyo watauona uso wake.


Ee BWANA, hakika mimi ni mtumishi wako, Mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako, Umevifungua vifungo vyangu.


BWANA huwalinda wasio na hila; Nilidhilika, akaniokoa.


Unigeukie na kunirehemu, Kama ilivyo desturi yako kwa walipendalo jina lako.


Wala usimhukumu mtumishi wako, Maana kwako hakuna aliye hai mwenye haki.


Ee Mungu, nimekuita kwa maana utaitika, Utege sikio lako ulisikie neno langu.


Mungu wangu, Mungu wangu, Mbona umeniacha? Mbona U mbali na wokovu wangu, Na maneno ya kuugua kwangu?


Atapokea baraka kwa BWANA, Na haki kwa Mungu wa wokovu wake.


Uniangalie na kunifadhili, Maana mimi ni mkiwa na mteswa.


Wala hukunitia mikononi mwa adui; Miguu yangu umeisimamisha mahali penye usalama.


Nami katika ukamilifu wangu umenitegemeza, Umeniweka mbele za uso wako milele.


Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu.


Moyo wangu umefurika kwa jambo jema, Mimi nasema niliyomfanyia mfalme; Ulimi wangu ni kama kalamu ya mwandishi stadi.


Mungu, unirehemu, maana yuko atakaye kunimeza, Mchana kutwa ananionea akileta vita.


Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi, Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe. Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako, Hadi misiba hii itakapopita.


BWANA, usinikemee kwa hasira yako, Wala usinirudi kwa ghadhabu yako.


Mungu na atufadhili na kutubariki, Na kutuangazia uso wake.


Katika Yuda Mungu amejulikana, Katika Israeli jina lake ni kuu.


Mmoja ataniambia, Kwa BWANA, peke yake, iko haki na nguvu; naam, watu watamwendea yeye, na wote waliomkasirikia watatahayarika.


Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, BWANA ni haki yetu.


MUNGU, aliye BWANA, ni nguvu zangu, Yeye huifanya miguu yangu kuwa kama ya kulungu, Naye ataniendesha katika mahali pangu palipoinuka.


Bali kwa yeye ninyi mmepata kuwa katika Kristo Yesu, aliyefanywa kwetu hekima itokayo kwa Mungu, na haki, na utakatifu, na ukombozi;


aliyetuokoa sisi katika mauti kuu namna ile; tena atatuokoa; ambaye tumemtumaini kuwa atazidi kutuokoa;


Maana ndugu, hatupendi, msijue habari ya dhiki ile iliyotupata katika Asia, ya kwamba tulilemewa mno kuliko nguvu zetu, hata tukakata tamaa ya kuishi.


Daudi akasema, BWANA aliyeniokoa na makucha ya simba, na makucha ya dubu, ataniokoa na mkono wa Mfilisti huyu. Sauli akamwambia Daudi, Nenda, na BWANA atakuwa pamoja nawe.