Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Zaburi 2:6 - Swahili Revised Union Version Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema “Nimemtawaza mfalme niliyemteua, anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!” Biblia Habari Njema - BHND “Nimemtawaza mfalme niliyemteua, anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!” Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza “Nimemtawaza mfalme niliyemteua, anatawala Siyoni, mlima wangu mtakatifu!” Neno: Bibilia Takatifu “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.” Neno: Maandiko Matakatifu “Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.” BIBLIA KISWAHILI Nami nimemweka mfalme wangu Juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu. |
Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele, Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza, Kuwa juu sana kuliko wafalme wote wa dunia.
Angalieni, nimemweka kuwa shahidi kwa makabila ya watu; kuwa kiongozi na jemadari kwa makabila ya watu.
Bwana MUNGU asema hivi; Mimi nami nitakitwaa kilele kirefu cha mwerezi, na kukipandikiza mahali; na katika vitawi vyake vilivyo juu nitatwaa kitawi kimoja kilicho chororo, nami nitakipanda juu ya mlima mrefu ulioinuka sana;
Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.
BWANA asema hivi, Mimi nimerudi Sayuni, nami nitakaa katikati ya Yerusalemu; na Yerusalemu utaitwa, Mji mwaminifu; na mlima wa BWANA wa majeshi utaitwa, mlima mtakatifu.
akavitia vitu vyote chini ya miguu yake, akamweka awe kichwa juu ya vitu vyote kwa ajili ya kanisa; ambalo
Bali ninyi mmeufikia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi,
Kisha nikaona, na tazama, huyo Mwana-kondoo amesimama juu ya mlima Sayuni, na watu elfu mia moja na arubaini na nne pamoja naye, wenye jina lake na jina la Baba yake limeandikwa katika vipaji vya nyuso zao.