Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 109:5 - Swahili Revised Union Version

Wamenilipa mabaya kwa mema yangu, Na chuki badala ya upendo wangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Wananilipa uovu kwa wema wangu, na chuki kwa mapendo yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Wananilipa uovu kwa wema wangu, na chuki kwa mapendo yangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Wananilipa uovu kwa wema wangu, na chuki kwa mapendo yangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Wananilipiza mabaya kwa mema, chuki badala ya urafiki wangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Wamenilipa mabaya kwa mema yangu, Na chuki badala ya upendo wangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 109:5
13 Marejeleo ya Msalaba  

Na walipotoka mjini, kabla hawajaendelea sana, Yusufu akamwambia yule msimamizi wa nyumba yake, Ondoka, uwafuate watu hawa, nawe utakapowapata, waambie, Kwa nini mmelipa mabaya kwa mema?


Absalomu alipokuwa akitoa dhabihu alituma Ahithofeli Mgiloni, Mshauri wake Daudi, aitwe kutoka mji wake, yaani, Gilo. Njama zao zikawa na nguvu; maana watu waliokuwa pamoja na Absalomu walizidi kuongezeka.


Mtu mmoja akamwambia Daudi ya kwamba, Ahithofeli yu katika hao waliopatana na Absalomu; Daudi akasema, Ee BWANA, nakusihi, uugeuze ushauri wa Ahithofeli uwe ubatili.


Naam, wakilipa mabaya kwa mema, Huwa adui zangu kwa kuwa nilifuata lililo jema.


Yeye arudishaye mabaya badala ya mema, Mabaya hayataondoka nyumbani mwake.


Je! Mabaya yalipwe badala ya mema? Maana wameichimbia nafsi yangu shimo. Kumbuka jinsi nilivyosimama mbele zako, ili niseme mema kwa ajili yao, nikaigeuze ghadhabu yako isiwapate.


na Yuda wa Yakobo, na Yuda Iskarioti, ndiye aliyekuwa msaliti.


Sisemi habari za ninyi nyote; nawajua wale niliowachagua; lakini andiko lipate kutimizwa, Aliyekula chakula changu Ameniinulia kisigino chake.


Kwa kuwa alihatarisha maisha yake, na kumpiga yule Mfilisti, naye BWANA akawatendea Israeli wote wokovu mkuu. Wewe mwenyewe uliona jambo hilo, ukafurahi; basi kwa nini kukosa juu ya damu isiyo na hatia, umwue huyo Daudi bure?