Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Yoshua 24:6 - Swahili Revised Union Version

Nikawatoa baba zenu watoke Misri; nanyi mkaifikia bahari; Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka Bahari ya Shamu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Niliwatoa wazee wenu kutoka Misri na kuwaleta hadi kwenye bahari ya Shamu. Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari na askari wapandafarasi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Niliwatoa wazee wenu kutoka Misri na kuwaleta hadi kwenye bahari ya Shamu. Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari na askari wapandafarasi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Niliwatoa wazee wenu kutoka Misri na kuwaleta hadi kwenye bahari ya Shamu. Wamisri waliwafuatia wakiwa na magari na askari wapandafarasi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nilipowatoa baba zenu Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari ya vita na wapanda farasi hadi Bahari ya Shamu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nilipowatoa baba zenu Misri, mlifika kwenye bahari, nao Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka kwenye Bahari ya Shamu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nikawatoa baba zenu watoke Misri; nanyi mkaifikia bahari; Wamisri wakawafuatia baba zenu kwa magari na wapanda farasi mpaka Bahari ya Shamu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Yoshua 24:6
11 Marejeleo ya Msalaba  

Nawe uliipasua bahari mbele yao, hata wakapita katikati ya bahari katika nchi kavu; na wale waliokuwa wakiwafuatia ukawatupa vilindini, kama jiwe katika maji makuu.


Aliipasua bahari akawavusha; Aliyafanya maji yasimame kama ukuta.


Wana wa Israeli wakasafiri kutoka Ramesesi mpaka Sukothi, walipata hesabu yao kama watu elfu mia sita wanaume waliokwenda kwa miguu, bila kuhesabu watoto.


Ilikuwa siku ile ile moja, BWANA akawatoa wana wa Israeli katika nchi ya Misri kwa majeshi yao.


Kwa maana nilikupandisha kutoka nchi ya Misri, na kukukomboa utoke katika nyumba ya utumwa, nami niliwatuma Musa, na Haruni, na Miriamu, watangulie mbele yako.


Huyo ndiye aliyewatoa, akifanya ajabu na ishara katika nchi ya Misri, na katika Bahari ya Shamu, na katika jangwa muda wa miaka arubaini.


Kwa imani wakapita kati ya Bahari ya Shamu, kama katika nchi kavu; Wamisri walipojaribu kufanya vivyo wakatoswa.