Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;
Tito 2:4 - Swahili Revised Union Version ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; Matoleo zaidiBiblia Habari Njema ili wawazoezeshe kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto, Biblia Habari Njema - BHND ili wawazoezeshe kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto, Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza ili wawazoezeshe kina mama vijana kuwapenda waume zao na watoto, Neno: Bibilia Takatifu ili waweze kuwafundisha wanawake vijana kuwa na kiasi, wawapende waume zao na kuwapenda watoto wao, Neno: Maandiko Matakatifu ili waweze kuwafundisha wanawake vijana kuwa na kiasi, wawapende waume zao na kuwapenda watoto wao, BIBLIA KISWAHILI ili wawatie wanawake vijana akili, wawapende waume zao, na kuwapenda watoto wao; |
Bali wajane walio vijana ukatae kuwaandika hao, maana, wakizidiwa na tamaa kinyume cha Kristo, wataka kuolewa;
Basi napenda wajane, ambao si wazee, waolewe, wazae watoto, watunze nyumba zao; ili wasimpe adui nafasi ya kulaumu.
Vivyo hivyo na wazee wa kike wawe na mwenendo wa utakatifu; wasiwe wasingiziaji, wasiwe wenye kutumia mvinyo nyingi, bali wanaofundisha yaliyo mema;
na kuwa wenye kiasi, kuwa safi, kufanya kazi nyumbani mwao, kuwa wema, kuwatii waume zao wenyewe; ili neno la Mungu lisitukanwe.