na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na linginelo lolote lisilopatana na mafundisho ya kweli;
Tito 2:1 - Swahili Revised Union Version Lakini wewe, nena mambo yanayoambatana na mafundisho mema; Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho sahihi. Biblia Habari Njema - BHND Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho sahihi. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Lakini wewe unapaswa kuhubiri mafundisho sahihi. Neno: Bibilia Takatifu Bali wewe fundisha yale yaliyo sahihi kulingana na mafundisho ya kweli. Neno: Maandiko Matakatifu Inakupasa kufundisha itikadi sahihi. BIBLIA KISWAHILI Lakini wewe, nena mambo yanayoambatana na mafundisho mema; |
na wazinifu, na wafiraji, na waibao watu, na waongo, nao waapao kwa uongo; na linginelo lolote lisilopatana na mafundisho ya kweli;
Mtu awaye yote akitoa mafundisho mengine, wala hayakubali maneno yenye uzima ya Bwana wetu Yesu Kristo, wala mafundisho yapatanayo na utauwa,
Shika mfano wa mafundisho ya kweli uliyoyasikia kwangu, katika imani na upendo ulio katika Kristo Yesu.
akilishika lile neno la imani vile vile kama alivyofundishwa, apate kuweza kuwaonya watu kwa mafundisho yenye uzima, na kuwashinda wenye kupinga.
Ni neno la kuaminiwa; na mambo hayo nataka uyasisitizie sana, ili wale waliomwamini Mungu wakumbuke kudumu katika matendo mema. Mambo hayo ni mazuri sana, tena yana manufaa kwa wanadamu.
Mtu akisema, na aseme kama asemaye maneno halisi ya Mungu; mtu akihudumu, na ahudumu kwa nguvu anazojaliwa na Mungu; ili Mungu atukuzwe katika mambo yote kwa Yesu Kristo. Utukufu na uweza una yeye hata milele na milele. Amina.