Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 24:19 - Swahili Revised Union Version

Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ole wao kina mama waja wazito na wanaonyonyesha siku hizo!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ole wao wenye mimba na wale wanaonyonyesha watoto siku hizo!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ole wao wenye mimba na wanyonyeshao siku hizo!

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 24:19
12 Marejeleo ya Msalaba  

Naye Yonathani, mwana wa Sauli alikuwa na mwana aliyekuwa na kilema cha miguu. Alikuwa na umri wa miaka mitano, habari za Sauli na Yonathani zilipofika Yezreeli, na yaya wake akamchukua akakimbia ikawa, alipokimbia kwa haraka, huyo mtoto akaanguka, akawa kilema. Na jina lake aliitwa Mefiboshethi.


Ndipo Menahemu akapiga Tifsa, na wote waliokuwamo, na mipaka yake, toka Tirza; kwa sababu hawakumfungulia, kwa hiyo akaupiga; nao wanawake wote waliokuwamo wenye mimba akawapasua.


Mikono ya wanawake wenye huruma Imewatokosa watoto wao wenyewe; Walikuwa ndio chakula chao Katika uharibifu wa binti ya watu wangu.


Samaria atachukua hatia yake; kwa maana amemwasi Mungu wake; wataanguka kwa upanga; watoto wao wachanga watavunjwa vipande vipande, na wanawake wao wenye mimba watatumbuliwa.


wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umejiandalia sifa?


wala aliye shambani asirudi nyuma kuichukua nguo yake.


Ombeni, ili kukimbia kwenu kusiwe wakati wa baridi, wala siku ya sabato.


Ole wao wenye mimba na wanaonyonyesha katika siku hizo! Kwa kuwa kutakuwa na shida nyingi katika nchi, na hasira juu ya taifa hili.