Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Mathayo 12:6 - Swahili Revised Union Version

Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko hekalu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko hekalu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Basi, nawaambieni kwamba hapa pana kikuu kuliko hekalu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nawaambia wazi kwamba, yeye aliye mkuu kuliko Hekalu yupo hapa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Lakini nawaambieni, kwamba hapa yupo aliye mkuu kuliko hekalu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Mathayo 12:6
12 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini Mungu je! Yamkini atakaa na watu duniani? Tazama, mbingu na mbingu za mbingu za mbingu hazikutoshi; seuze nyumba hii niliyoijenga!


BWANA asema hivi, Mbingu ni kiti changu cha enzi, na dunia ni mahali pa kuweka miguu yangu; mtanijengea nyumba ya namna gani? Na mahali pangu pa kupumzikia ni mahali gani?


Maana mkono wangu ndio uliofanya hivi vyote, vitu hivi vyote vikapata kutokea, asema BWANA; lakini mtu huyu ndiye nitakayemwangalia, mtu aliye mnyonge, mwenye roho iliyopondeka, atetemekaye asikiapo neno langu.


Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijia katika hekalu lake ghafla; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema BWANA wa majeshi.


Wala hamkusoma katika torati, kwamba siku ya sabato makuhani hekaluni huinajisi sabato pasipo kupata hatia?


Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.