Siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yoyote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.
Hesabu 28:25 - Swahili Revised Union Version Na siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yoyote ya utumishi. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Katika siku ya saba mtafanya mkutano mtakatifu; msifanye kazi. Biblia Habari Njema - BHND Katika siku ya saba mtafanya mkutano mtakatifu; msifanye kazi. Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Katika siku ya saba mtafanya mkutano mtakatifu; msifanye kazi. Neno: Bibilia Takatifu Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida. Neno: Maandiko Matakatifu Siku ya saba mwe na kusanyiko takatifu na msifanye kazi zenu za kawaida. BIBLIA KISWAHILI Na siku ya saba mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yoyote ya utumishi. |
Siku ya kwanza kutakuwa kwenu na kusanyiko takatifu, na siku ya saba kutakuwa kusanyiko takatifu; haitafanywa kazi yoyote katika siku hizo, isipokuwa kwa hiyo ambayo kila mtu hana budi kula, hiyo tu ifanyike kwenu.
Mtakula mikate isiyochachwa muda wa siku saba, nayo siku ya saba itakuwa ni sikukuu ya BWANA.
Nanyi mtatangaza suku iyo hiyo; kutakuwa na kusanyiko takatifu kwenu; msifanye kazi yoyote ya utumishi; ni amri ya milele katika makao yenu yote, katika vizazi vyenu.
Mtafanya kazi siku sita; lakini siku ya saba ni Sabato ya kustarehe kabisa, kusanyiko takatifu; msifanye kazi ya namna yoyote; ni Sabato kwa BWANA katika makao yenu yote.
Lakini mtasongeza sadaka kwa BWANA kwa njia ya moto siku saba; siku ya saba ni kusanyiko takatifu; msifanye kazi yoyote ya utumishi.
Tena katika siku ya malimbuko, hapo mtakapomsogezea BWANA sadaka ya unga mpya katika sikukuu yenu ya majuma mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yoyote ya utumishi;
Tena mwezi wa saba, siku ya kwanza ya mwezi, mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yoyote ya utumishi; ni siku ya kupiga tarumbeta kwenu.
Tena siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba mtakuwa na kusanyiko takatifu; hamtafanya kazi yoyote kwenye nafsi zenu, nanyi mtamfanyia BWANA sikukuu muda wa siku saba;
Tena siku ya nane mtakuwa na kusanyiko la makini sana; hamtafanya kazi yoyote kwenye nafsi zenu;
Siku sita utakula mikate isiyotiwa chachu; na siku ya saba na uwe mkutano mtukufu kwa BWANA, Mungu wako, usifanye kazi yoyote.