Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Hesabu 19:15 - Swahili Revised Union Version

Na kila chombo kilicho wazi, kisichofungwa na kifuniko, ni najisi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kila chombo kilicho wazi ambacho hakina kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kila chombo kilicho wazi ambacho hakina kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kila chombo kilicho wazi ambacho hakina kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

nacho kila chombo kisicho na kifuniko juu yake kitakuwa najisi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Na kila chombo kilicho wazi, kisichofunikwa na kifuniko, ni najisi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Hesabu 19:15
6 Marejeleo ya Msalaba  

Tena kitu chochote, wanyama hao mmojawapo atakachokiangukia, wakiisha kufa, kitakuwa ni najisi; cha mti, nguo, ngozi, gunia, chombo chochote cha kufanyia kazi yoyote, lazima kitiwe ndani ya maji, nacho kitakuwa ni najisi hadi jioni; ndipo kitakapokuwa ni safi.


Na kila chombo cha udongo, wanyama hao mmojawapo atakachokiangukia, kila kilichomo ndani yake kitakuwa ni najisi, na hicho chombo kitavunjwa.


ndipo kuhani ataagiza kwamba watoe vyote vilivyomo nyumbani, kabla kuhani hajaingia ndani kuliangalia hilo pigo, ili vyote vilivyomo nyumbani visiwe najisi, kisha baadaye kuhani ataingia ndani ya nyumba hiyo aikague;


Hii ndiyo amri, mtu afapo ndani ya hema; kila mtu aingiaye ndani ya hema hiyo, na kila mtu aliye humo hemani, atakuwa najisi muda wa siku saba.


Kisha mtu yeyote huko nje shambani atakayemgusa mtu aliyeuawa kwa upanga, au mzoga, au mfupa wa mtu, au kaburi, atakuwa najisi muda wa siku saba.


Na kuhusu kila nguo, na kila kitu kilichofanywa cha ngozi, na kazi yote ya singa za mbuzi, na vyombo vyote vilivyofanywa vya mti, mtajitakasa wenyewe;