Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zekaria 9:14 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Naye BWANA ataonekana juu yao, Na mshale wake utatoka kama umeme; Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta, Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwenyezi-Mungu atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana Mwenyezi-Mungu atapiga tarumbeta; atafika pamoja na kimbunga cha kusini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwenyezi-Mungu atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana Mwenyezi-Mungu atapiga tarumbeta; atafika pamoja na kimbunga cha kusini.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwenyezi-Mungu atawatokea watu wake; atafyatua mishale yake kama umeme. Bwana Mwenyezi-Mungu atapiga tarumbeta; atafika pamoja na kimbunga cha kusini.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Kisha Mwenyezi Mungu atawatokea; mshale wake utamulika kama radi. Bwana Mungu Mwenyezi atapiga tarumbeta, naye atatembea katika tufani za kusini,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Kisha bwana atawatokea; mshale wake utamulika kama umeme wa radi. bwana Mwenyezi atapiga tarumbeta, naye atatembea katika tufani za kusini,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Naye BWANA ataonekana juu yao, Na mshale wake utatoka kama umeme; Na Bwana MUNGU ataipiga tarumbeta, Naye atakwenda kwa pepo za kisulisuli za kusini.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zekaria 9:14
28 Marejeleo ya Msalaba  

Dhoruba hutoka katika vyumba vyake; Na baridi ghalani mwake.


Akaipiga mishale yake akawatawanya, Naam, umeme mwingi sana, akawatapanya.


Ndipo ilipoonekana mikondo ya maji, Misingi ya ulimwengu ikafichuliwa, Ee BWANA, kwa kukemea kwako, Kwa mvumo wa pumzi ya puani mwako.


Enyi watu mkaao katika ulimwengu wote, na wenyeji wa dunia, bendera ikiinuliwa milimani, angalieni; na wakipiga tarumbeta, sikieni.


Ufunuo juu ya nyika kando ya bahari. Kama tufani za Negebu zikaribiavyo kwa kasi, inakuja kutoka kwa nyika, toka nchi itishayo.


Tena itakuwa katika siku hiyo, tarumbeta kubwa itapigwa, nao waliokuwa karibu kuangamia katika nchi ya Ashuru watakuja; na hao waliotupwa katika nchi ya Misri; nao watamsujudu BWANA katika mlima mtakatifu huko Yerusalemu.


Naye BWANA atawasikizisha watu sauti yake ya utukufu, naye atawaonesha jinsi mkono wake ushukavyo, na ghadhabu ya hasira yake, na mwako wa moto uangamizao, pamoja na dhoruba, na tufani, na mvua ya mawe ya barafu.


Kama ndege warukao, BWANA wa majeshi ataulinda Yerusalemu; ataulinda na kuuokoa, atapita juu yake na kuuhifadhi.


Maana BWANA atakuja na moto, na magari yake ya vita kama upepo wa kisulisuli; ili atoe malipo ya ghadhabu yake kwa moto uwakao, na maonyo yake kwa miali ya moto.


Jua na mwezi vikasimama makaoni mwao; Mbele ya nuru ya mishale yako ilipotapakaa, Mbele ya mwangaza wa mkuki wako umeremetao.


Ukakichoma kichwa cha mashujaa wake kwa fimbo zao wenyewe; Wakaja kama kisulisuli ili kunitawanya; Kama wakifurahi kuwameza maskini kwa siri.


Katika siku hiyo BWANA atawalinda wenyeji wa Yerusalemu; na yeye aliye dhaifu miongoni mwao atakuwa kama Daudi siku hiyo; nayo nyumba ya Daudi itakuwa kama Mungu, kama malaika wa BWANA mbele yao.


Hapo ndipo atakapotokea BWANA, naye atapigana na mataifa hayo, kama anavyopigana siku ya vita.


Kwa maana mimi, asema BWANA, nitakuwa ukuta wa moto kuuzunguka pande zote, nami nitakuwa huo utukufu ndani yake.


Naye atawatuma malaika wake pamoja na sauti kuu ya parapanda, nao watawakusanya wateule wake toka pepo nne, toka mwisho huu wa mbingu mpaka mwisho huu.


na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi; na tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.


kwa nguvu za ishara na maajabu, katika nguvu za Roho Mtakatifu; hata ikawa tangu Yerusalemu, na kandokando yake, mpaka Iliriko nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa utimilifu;


Mungu naye akishuhudia pamoja nao kwa ishara na ajabu na nguvu za namna nyingi, na kwa karama za Roho Mtakatifu, kama alivyopenda mwenyewe.


Na wafalme hao wote na nchi zao Yoshua akatwaa kwa wakati mmoja, kwa sababu yeye BWANA, Mungu wa Israeli, alipigana kwa ajili ya Israeli,


Nikaona, na tazama, farasi mweupe, na yeye aliyempanda ana uta, akapewa taji, naye akatoka, huku akishinda tena apate kushinda.