Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 96:8 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mpeni BWANA utukufu wa jina lake, Leteni sadaka, na mwingie katika nyua zake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Lisifuni jina lake tukufu; leteni tambiko na kuingia hekaluni mwake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Lisifuni jina lake tukufu; leteni tambiko na kuingia hekaluni mwake.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Lisifuni jina lake tukufu; leteni tambiko na kuingia hekaluni mwake.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mpeni Mwenyezi Mungu utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mpeni bwana utukufu unaostahili jina lake; leteni sadaka na mje katika nyua zake.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mpeni BWANA utukufu wa jina lake, Leteni sadaka, na mwingie katika nyua zake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 96:8
21 Marejeleo ya Msalaba  

Ingieni malangoni mwake kwa shukrani; Nyuani mwake kwa kusifu; Mshukuruni, lihimidini jina lake;


Amewapelekea watu wake ukombozi, Ameamuru agano lake liwe la milele, Jina lake ni takatifu na la kuogopwa.


Katika nyua za nyumba ya BWANA, Ndani yako, Ee Yerusalemu.


Mpeni BWANA utukufu wa jina lake; Mwabuduni BWANA kwa uzuri wa utakatifu.


Na watu wa Tiro wanakushawishi kwa zawadi, Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.


Wafalme wa Tarshishi na visiwa na walete kodi; Wafalme wa Sheba na Seba na watoe vipawa.


Watu wa nchi nao wataabudu mbele ya mlango wa lile lango mbele za BWANA, siku za sabato, na siku za mwezi mwandamo.


Kwa maana tokea maawio ya jua hata machweo yake jina langu ni kuu katika mataifa; na katika kila mahali unatolewa uvumba na dhabihu safi kwa jina langu; maana jina langu ni kuu katika mataifa, asema BWANA wa majeshi.


Basi, ndugu zangu, nawasihi, kwa huruma zake Mungu, itoeni miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, ya kumpendeza Mungu, ndiyo ibada yenu yenye maana.


ili niwe mhudumu wa Kristo Yesu kati ya watu wa Mataifa, niifanyie Injili ya Mungu kazi ya ukuhani, kusudi Mataifa wawe sadaka yenye kibali, ikiisha kutakaswa na Roho Mtakatifu.


Naam, hata nikimiminwa juu ya dhabihu na ibada ya imani yenu, nafurahi; tena nafurahi pamoja nanyi nyote.


Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafrodito vitu vile vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.


Basi na tutoke tumwendee nje ya kambi, tukichukua shutuma yake.


Ninyi nanyi, kama mawe yaliyo hai, mmejengwa muwe nyumba ya Roho, ukuhani mtakatifu, mtoe dhabihu za roho, zinazokubaliwa na Mungu, kwa njia ya Yesu Kristo.


Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu; kwa maana mataifa yote watakuja na kusujudu mbele zako; kwa kuwa matendo yako ya haki yamekwisha kufunuliwa.