Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 96:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mwimbieni BWANA, lisifuni jina lake, Tangazeni wokovu wake kila siku.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mwimbieni Mwenyezi-Mungu na kulisifu jina lake. Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mwimbieni Mwenyezi-Mungu na kulisifu jina lake. Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mwimbieni Mwenyezi-Mungu na kulisifu jina lake. Tangazeni kila siku matendo yake ya wokovu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwimbieni Mwenyezi Mungu, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwimbieni bwana, lisifuni jina lake; tangazeni wokovu wake siku baada ya siku.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mwimbieni BWANA, lisifuni jina lake, Tangazeni wokovu wake kila siku.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 96:2
16 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Daudi akawaambia kusanyiko lote, Haya, mhimidini BWANA, Mungu wenu. Basi kusanyiko lote wakamhimidi BWANA, Mungu wa baba zao, wakainamisha vichwa vyao, wakamsujudia BWANA, na mfalme naye.


Mhimidini BWANA, enyi malaika zake, Ninyi mlio hodari, mtendao neno lake, Mkiisikiliza sauti ya neno lake.


Ee Mungu wangu, Mfalme, nitakutukuza, Nitalihimidi jina lako milele na milele.


Ee BWANA, kazi zako zote zitakushukuru, Na wacha Mungu wako watakuhimidi.


Kila siku nitakuhimidi, Nitalisifu jina lako milele na milele.


Sikusitiri haki yako moyoni mwangu; Nimetangaza uaminifu wako na wokovu wako. Sikuficha fadhili zako wala kweli yako Katika kusanyiko kubwa.


Lakini mimi nitakutumainia daima Na nitaendelea kukusifu zaidi na zaidi.


Wewe uuhubiriye Sayuni habari njema, Panda juu ya mlima mrefu; Wewe uuhubiriye Yerusalemu habari njema, Paza sauti kwa nguvu; Paza sauti yako, usiogope; Iambie miji ya Yuda, Tazameni, Mungu wenu.


Akawaambia, Nendeni ulimwenguni kote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.


Ndugu zangu, wana wa ukoo wa Abrahamu, na hao miongoni mwenu wanaomcha Mungu, kwetu sisi neno la wokovu huu limepelekwa.


Atukuzwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, aliyetubariki kwa baraka zote za rohoni, katika ulimwengu wa roho, ndani yake Kristo;


Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi na juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nilivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na kwake Mwana-kondoo, hata milele na milele.