Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 95:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Njoni, tumwimbie BWANA, Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu, tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu, tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Njoni tumwimbie Mwenyezi-Mungu, tumshangilie mwamba wa wokovu wetu!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Njooni, tumwimbie Mwenyezi Mungu kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Njooni, tumwimbie bwana kwa furaha; tumfanyie kelele za shangwe Mwamba wa wokovu wetu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Njoni, tumwimbie BWANA, Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 95:1
36 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA yu hai; Na ahimidiwe mwamba wangu; Na atukuzwe Mungu wangu, mwamba wa wokovu wangu;


Mwimbieni, mwimbieni nyimbo za kumsifu; Yatangazeni matendo yake yote ya ajabu.


Wakafika Yerusalemu wenye vinanda, vinubi na parapanda kwenda nyumbani kwa BWANA.


Mshangilieni BWANA, enyi nchi zote;


Rehema na hukumu nitaziimba, Ee BWANA, nitakuimbia zaburi.


Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Na wamshukuru BWANA, kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Haleluya. Enyi mataifa yote, msifuni BWANA, Enyi watu wote, mhimidini.


Haleluya. Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema, Kwa maana fadhili zake ni za milele.


Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA. Haleluya.


Ndiye Mungu anilipizaye kisasi; Na kuwatiisha watu chini yangu.


Mtukuzeni BWANA pamoja nami, Na tuliadhimishe jina lake pamoja.


Enyi mataifa, mtukuzeni Mungu wetu, Itangazeni sauti ya sifa zake;


Mwimbieni Mungu, nguvu zetu, nyimbo za furaha, Mshangilieni Mungu wa Yakobo.


Yeye ataniita, Wewe ni baba yangu, Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.


Ndipo Musa na wana wa Israeli wakamwimbia BWANA wimbo huu wakanena, na kusema, Nitamwimbia BWANA, kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.


Miriamu akawaitikia, Mwimbieni BWANA kwa maana ametukuka sana; Farasi na mpanda farasi amewatupa baharini.


itasikika tena sauti ya furaha na sauti ya shangwe, sauti ya bwana arusi na sauti ya bibi arusi, sauti yao wasemao Mshukuruni BWANA wa majeshi, maana BWANA ni mwema, rehema zake ni za milele; na sauti zao waletao sadaka za shukrani nyumbani kwa BWANA. Kwa kuwa nitawarudisha wafungwa wa nchi hii kama kwanza, asema BWANA.


Na makutano waliotangulia, na wale waliofuata, wakapaza sauti, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi; ndiye mbarikiwa, yeye ajaye kwa jina la Bwana; Hosana juu mbinguni.


wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo.


mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;


Lakini Yeshuruni alinenepa, akapiga teke; Umenenepa, umekuwa mnene, umewanda; Ndipo akamwacha Mungu aliyemfanya, Akamdharau Mwamba wa wokovu wake.


Neno la Kristo na likae kwa wingi ndani yenu katika hekima yote, mkifundishana na kuonyana kwa zaburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni; huku mkimwimbia Mungu kwa neema mioyoni mwenu.


na kuimba wimbo mpya mbele ya kile kiti cha enzi, na mbele ya wale wenye uhai wanne, na wale wazee; wala hakuna mtu aliyeweza kujifunza wimbo ule, ila wale elfu mia moja na arubaini na nne, walionunuliwa katika nchi.


Nao wauimba wimbo wa Musa, mtumwa wa Mungu, na wimbo wa Mwana-kondoo, wakisema, Ni makuu, na ya ajabu, matendo yako, Ee Bwana Mungu Mwenyezi; Ni za haki, na za kweli, njia zako, Ee Mfalme wa mataifa.


Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi, na kama sauti ya maji mengi, na kama sauti ya radi yenye nguvu, ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki.


Nao waimba wimbo mpya wakisema, Wastahili wewe kukitwaa hicho kitabu na kuifungua mihuri yake; kwa kuwa ulichinjwa, ukawa fidia kwa Mungu na kwa damu yako watu wa kila kabila na lugha na jamaa na taifa,