Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 92:7 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Hata wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakastawi. Mwishowe wataangamizwa milele;

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kwamba waovu waweza kustawi kama nyasi, watenda maovu wote waweza kufanikiwa, lakini mwisho wao ni kuangamia milele,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kwamba waovu waweza kustawi kama nyasi, watenda maovu wote waweza kufanikiwa, lakini mwisho wao ni kuangamia milele,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

kwamba waovu waweza kustawi kama nyasi, watenda maovu wote waweza kufanikiwa, lakini mwisho wao ni kuangamia milele,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao maovu wanastawi, wataangamizwa milele.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

ingawa waovu huchipua kama majani na wote watendao mabaya wanastawi, wataangamizwa milele.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Hata wasio haki wakichipuka kama majani Na wote watendao maovu wakastawi. Mwishowe wataangamizwa milele;

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 92:7
21 Marejeleo ya Msalaba  

Hema za wanyang'anyi hufanikiwa, Na hao wamkasirishao Mungu hukaa salama; Mikononi mwao Mungu huleta vitu vingi.


Wakosaji wataangamizwa pamoja, Wasio haki mwisho wao wataharibiwa.


Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.


Nilikuwa kama mjinga, sijui neno; Nilikuwa kama mnyama tu mbele zako.


Je! Wote watendao uovu watatoa maneno, Na kusema majivuno, na kufanya kiburi?


Maana kurudi nyuma kwao wajinga kutawaua, Na kufanikiwa kwao wapumbavu kutawaangamiza.


Ndiyo sababu wenyeji wao wakawa hawana nguvu, na kufadhaika, na kuhangaika, wakawa kama majani ya mashamba, kama miche mibichi, kama majani juu ya madari, kama shamba la ngano kabla haijaiva.


Na sasa twasema ya kwamba wenye kiburi ndio walio heri; naam, watendao uovu ndio wajengwao; naam, wamjaribuo Mungu ndio waponywao.


Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuri; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi.


Maana, Mwili wote ni kama majani, Na fahari yake yote ni kama ua la majani. Majani hukauka na ua lake huanguka;