Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 89:24 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Nitakuwa mwaminifu kwake na kumfadhili, kwa jina langu atapata ushindi mkubwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Nitakuwa mwaminifu kwake na kumfadhili, kwa jina langu atapata ushindi mkubwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Nitakuwa mwaminifu kwake na kumfadhili, kwa jina langu atapata ushindi mkubwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Upendo wangu mkamilifu utakuwa pamoja naye, kwa Jina langu pembe yake itatukuzwa.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo, Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 89:24
15 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akujibu siku ya dhiki, Jina la Mungu wa Yakobo likuinue.


Na tuushangilie wokovu wako, Kwa jina la Mungu wetu tuzitweke bendera zetu. BWANA akutimizie matakwa yako yote.


Atakaa mbele za Mungu milele, Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.


Hata milele nitamwekea fadhili zangu, Na agano langu naye litadumu hata milele.


Lakini fadhili zangu sitamwondolea yeye, Wala sitafanya uaminifu wangu kuwa uongo.


Kwa kuwa amekaza kunipenda Nitamwokoa; na kumweka palipo juu, Kwa kuwa amenijua Jina langu.


Kwa kuwa torati ilitolewa kwa mkono wa Musa; neema na kweli zilikuja kwa mkono wa Yesu Kristo.


Wala mimi simo tena ulimwenguni, lakini hawa wamo ulimwenguni, nami naja kwako. Baba mtakatifu, kwa jina lako ulilonipa uwalinde hawa, ili wawe na umoja kama sisi tulivyo.


Nami niliwajulisha jina lako, tena nitawajulisha hilo; ili pendo lile ulilonipenda mimi liwe ndani yao, nami niwe ndani yao.


Jina lako nimewadhihirishia watu wale ulionipa katika ulimwengu; walikuwa wako, ukanipa mimi, na neno lako wamelishika.


Maana ahadi zote za Mungu zilizopo katika yeye ni Ndiyo; tena kwa hiyo katika yeye ni Amin; Mungu apate kutukuzwa kwa sisi.


Na baraka ya Yuda ni hii; akasema, Isikize, Ee BWANA, sauti ya Yuda, Umlete ndani kwa watu wake; Alijitetea kwa mikono yake; Nawe utakuwa msaada juu ya adui zake.


Naye Hana akaomba, akasema, Moyo wangu wamshangilia BWANA, Pembe yangu imetukuka katika BWANA, Kinywa changu kimepanuka juu ya adui zangu; Kwa kuwa naufurahia wokovu wako;