Zaburi 82:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Mungu anasimamia baraza lake; anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu: Biblia Habari Njema - BHND Mungu anasimamia baraza lake; anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu: Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Mungu anasimamia baraza lake; anatoa hukumu katika kusanyiko la miungu: Neno: Bibilia Takatifu Mungu anaongoza kusanyiko kuu, anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”: Neno: Maandiko Matakatifu Mungu anaongoza kusanyiko kuu, anatoa hukumu miongoni mwa “miungu”: BIBLIA KISWAHILI Mungu asimama katika kusanyiko la Mungu; Katikati ya miungu anahukumu. |
Na mwanadamu atasema, Hakika iko thawabu yake mwenye haki. Hakika yuko Mungu Anayehukumu katika dunia.
Zaidi ya hayo utajipatia katika watu hawa watu walio na uwezo, wenye kumcha Mungu, watu wa kweli, wenye kuchukia mapato ya udhalimu; ukawaweka juu yao, wawe wakuu wa maelfu, na wakuu wa mamia, na wakuu wa hamsini hamsini, na wakuu wa kumi kumi;
ndipo hapo huyo bwana wake atamleta mbele ya Mungu na kumleta mlangoni, au penye mwimo wa mlango; na bwana wake atalitoboa sikio lake kwa uma; ndipo atamtumikia sikuzote.
Ujapokuwa unaona maskini kuonewa, na hukumu na haki kuondolewa kwa jeuri katika jimbo, usilistaajabie jambo hilo; kwa sababu, Aliye Juu kuliko walio juu huangalia; Tena wako walio juu kupita hao.
Ikiwa aliwaita miungu wale waliojiwa na neno la Mungu; (na maandiko hayawezi kutanguka);