Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 81:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hivyo, nikawaacha wabaki na ukaidi wao; wafuate mashauri yao wenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hivyo, nikawaacha wabaki na ukaidi wao; wafuate mashauri yao wenyewe.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hivyo, nikawaacha wabaki na ukaidi wao; wafuate mashauri yao wenyewe.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Basi niliwaacha katika ukaidi wa mioyo yao wafuate mashauri yao wenyewe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nikawaacha wakaenda kwa ukaidi wa mioyo yao, Waenende katika mashauri yao.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 81:12
20 Marejeleo ya Msalaba  

BWANA akasema, Roho yangu haitashindana na mwanadamu milele, kwa kuwa yeye naye ni mwili; basi siku zake zitakuwa miaka mia moja na ishirini.


kwa sababu hawakuitii sauti ya BWANA, Mungu wao, bali waliyavunja maagano yake, mambo yote ambayo Musa mtumishi wa BWANA aliwaamuru, wasikubali kuyasikiliza, wala kuyatenda.


Lakini wao na baba zetu wakatakabari, wakafanya shingo zao kuwa ngumu, wala hawakuzisikiliza amri zako,


Kwamba watoto wako wamemfanyia dhambi, Naye amewatia mkononi mwa kosa lao;


BWANA akamwambia Musa, Farao hatawasikiza ninyi; kusudi ajabu zangu ziongezeke katika nchi ya Misri.


Ole wa watoto waasi; asema BWANA; watakao mashauri lakini hawayataki kwangu mimi; wajifunikao kifuniko lakini si cha roho yangu; wapate kuongeza dhambi juu ya dhambi;


Kwa maana watu hawa ni watu waasi, watoto wasemao uongo, watoto wasiotaka kuisikia sheria ya BWANA;


Ni nani aliyemtoa Yakobo awe mateka, aliyemtia Israeli katika mikono ya wanyang'anyi? Si yeye, BWANA? Yeye tuliyemkosea, ambaye hawakutaka kwenda katika njia zake, wala hawakuitii sheria yake.


nami nimewafunulia haya leo; lakini ninyi hamkuitii sauti ya BWANA, Mungu wenu, katika neno lolote ambalo amenituma kwenu.


Lakini hawakusikiliza, wala kutega sikio lao, bali walikwenda kwa mashauri yao wenyewe, na kwa ushupavu wa mioyo yao mibaya, wakaenda nyuma wala si mbele.


Lakini waliniasi, wala hawakutaka kunisikiliza; hawakutupilia mbali kila mtu machukizo ya macho yake, wala hawakuviacha vinyago vya Misri; ndipo nikasema kwamba nitamwaga ghadhabu yangu juu yao, ili kuitimiza hasira yangu juu yao, katikati ya nchi ya Misri.


Mungu wangu atawatupilia mbali, kwa sababu hawakumsikiliza; nao watakuwa watu wa kutangatanga kati ya mataifa.


Lakini msiponisikiza, wala hamtaki kuyafanya maagizo hayo yote;


ambaye zamani zilizopita aliwaacha mataifa yote waende katika njia zao wenyewe.


Basi Mungu akaghairi, akawaacha ili waliabudu jeshi la mbinguni, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha manabii, Je! Mlinitolea mimi dhabihu na sadaka Miaka arubaini katika jangwa, enyi nyumba ya Israeli?


Kwa ajili ya hayo Mungu aliwaacha katika tamaa za mioyo yao, waufuate uchafu, hata wakavunjiana heshima miili yao.


Lakini hao watu wakakataa kuisikiliza sauti ya Samweli; wakasema, Sivyo hivyo; lakini tunataka kuwa na mfalme juu yetu;