Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 80:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ee BWANA, Mungu wa majeshi, hadi lini Utayaghadhibikia maombi ya watu wako?

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi, hata lini utazikasirikia sala za watu wako?

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi, hata lini utazikasirikia sala za watu wako?

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Ee Mwenyezi-Mungu, Mungu wa majeshi, hata lini utazikasirikia sala za watu wako?

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Bwana Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni, hata lini hasira yako itawaka dhidi ya maombi ya watu wako?

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote, hata lini hasira yako itawaka na kufoka moshi dhidi ya maombi ya watu wako?

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee BWANA, Mungu wa majeshi, hadi lini Utayaghadhibikia maombi ya watu wako?

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 80:4
14 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, nisiaibishwe, maana nimekuita; Waaibishwe wasio haki, wanyamaze kuzimuni.


Umenitia furaha moyoni mwangu, Kupita yao wanapozidishiwa nafaka na divai.


Na Wewe, BWANA, Mungu wa majeshi, Mungu wa Israeli, uinuke. Uwapatilize mataifa yote; Usimrehemu hata mmoja wa wale wapangao maovu kwa hila.


Umewaonesha watu wako mazito, Na kutunywesha mvinyo ya kutuyumbisha.


Ee Mungu, mbona umetutupa milele? Kwa nini hasira yako inatoka moshi Juu ya kondoo wa malisho yako?


Ee BWANA, hadi lini? Utaona hasira milele? Wivu wako utawaka kama moto?


Je! Utatufanyia hasira hata milele? Utadumisha ghadhabu kizazi hadi kizazi?


Umejifunika nafsi yako kwa wingu, Maombi yetu yasipite.


Basi sasa, Ee Mungu wetu, yasikilize maombi ya mtumishi wako, na dua zake, ukaangazishe uso wako juu ya patakatifu pako palipo ukiwa, kwa ajili ya Bwana.


BWANA hatamsamehe mtu huyo, lakini wakati huo hasira ya BWANA na wivu wake vitafuka moshi juu ya mtu yule, na laana yote iliyoandikwa katika kitabu hiki itamkalia juu yake, na BWANA atalifuta jina lake chini ya mbingu.