Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 79:6 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ukali wako uwamwagie mataifa wasiokujua, Na falme za hao wasioliitia jina lako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Uwamwagie watu wasiokujua hasira yako; naam, tawala zote zisizoheshimu jina lako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Uwamwagie watu wasiokujua hasira yako; naam, tawala zote zisizoheshimu jina lako.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Uwamwagie watu wasiokujua hasira yako; naam, tawala zote zisizoheshimu jina lako.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali, juu ya falme za hao wasioliitia jina lako,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Mwaga ghadhabu yako kwa mataifa yasiyokukubali, juu ya falme za hao wasioliitia jina lako,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ukali wako uwamwagie mataifa wasiokujua, Na falme za hao wasioliitia jina lako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 79:6
22 Marejeleo ya Msalaba  

Je! Wote wafanyao maovu hawajui? Walao watu wangu kama walavyo mkate, Hawamwiti BWANA.


BWANA yuko karibu na wote wamwitao, Wote wamwitao kwa uaminifu.


Je! Wafanyao maovu hawajui? Walao watu wangu kama walavyo mkate, Hawakumwita MUNGU.


Uimwage ghadhabu yako juu yao, Na ukali wa hasira yako uwapate.


Kwa sababu hiyo alimwaga ukali wa hasira yake juu yake, na nguvu za vita; ukawasha moto wa kumzunguka pande zote, wala hakujua; ukamteketeza, wala hakuyatia hayo moyoni mwake.


Hasira yako uwamwagie mataifa wasiokujua, na jamaa zao wasioliitia jina lako; kwa maana wamemla Yakobo, naam, wamemla kabisa na kumwangamiza, na kuyafanya makao yake kuwa ukiwa.


Maana angalieni, ninaanza kutenda mabaya katika mji uitwao kwa jina langu, je! Mtaachiliwa ninyi msiadhibiwe? Hamtaachiliwa msiadhibiwe; kwa maana nitauita upanga ule uwapige wote wakaao katika dunia, asema BWANA wa majeshi.


Basi ningojeeni, asema BWANA, hata siku ile nitakapoondoka kuteka mateka; maana nimeazimia kuwakusanya mataifa, ili nizikutanishe falme, nipate kuwamwagia ghadhabu yangu; naam, ukali wote wa hasira yangu; kwa maana dunia yote itateketezwa kwa moto wa wivu wangu.


Na hayo watawatenda kwa sababu hawakumjua Baba wala mimi.


Baba mwenye haki, ulimwengu haukukujua; lakini mimi nilikujua, na hao wamejua ya kuwa ndiwe uliyenituma.


Kwa sababu nilipokuwa nikipita huku na huko na kuyaona mambo ya ibada yenu, niliona madhabahu iliyoandikwa maneno haya, KWA MUNGU ASIYEJULIKANA. Basi mimi nawahubirini habari zake yeye ambaye ninyi mnamwabudu bila kumjua.


Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa, wayafanye yasiyowapasa.


kwa kanisa la Mungu lililoko Korintho, wale waliotakaswa katika Kristo Yesu, walioitwa wawe watakatifu, pamoja na wote wanaoliitia jina la Bwana wetu Yesu Kristo kila mahali, Bwana wao na wetu.


katika muali wa moto; huku akiwalipiza kisasi wao wasiomjua Mungu, na wao wasioitii Injili ya Bwana wetu Yesu;