Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 78:61 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Aliiacha ishara ya nguvu yake itekwe, utukufu wake utiwe mikononi mwa maadui.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Aliiacha ishara ya nguvu yake itekwe, utukufu wake utiwe mikononi mwa maadui.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Aliiacha ishara ya nguvu yake itekwe, utukufu wake utiwe mikononi mwa maadui.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Akalipeleka Sanduku la nguvu zake utumwani, utukufu wake mikononi mwa adui.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Akaziacha nguvu zake kutekwa, Na fahari yake mkononi mwa mtesi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 78:61
10 Marejeleo ya Msalaba  

Sasa, Ee BWANA, Mungu, uondoke, uende kwenye raha yako, wewe na sanduku la nguvu zako; makuhani wako, Ee BWANA, Mungu, wavikwe wokovu, watakatifu wako na washangilie mema.


Ee BWANA, uinuke, uende kwenye raha yako, Wewe na sanduku la nguvu zako.


Inueni vichwa vyenu, enyi malango, Inukeni, enyi malango ya milele, Mfalme wa utukufu apate kuingia.


Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu, Nizione nguvu zako na utukufu wako.


Ndipo lile wingu likaifunikiza hema ya kukutania, na huo utukufu wa BWANA ukaijaza maskani.


Kisha wana wa Dani wakajisimamishia hiyo sanamu ya kuchonga; na Yonathani mwana wa Gershomu, mwana wa Musa, yeye na wanawe walikuwa ni makuhani katika kabila la Wadani hadi siku nchi hiyo ilipochukuliwa mateka.


Yeye aliyeleta habari akajibu, akasema, Israeli wamekimbia mbele ya Wafilisti, tena watu wengi sana wameuawa, hata na wana wako wawili, Hofni na Finehasi, wamekufa pia, na sanduku la Mungu limetwaliwa.


Akamwita mtoto, Ikabodi, akisema, Huo utukufu umeondoka katika Israeli; kwa sababu sanduku la Mungu lilikuwa limetwaliwa, na kwa sababu ya mkwewe na mumewe.


Basi, hilo sanduku la BWANA lilikuwamo katika nchi ya Wafilisti muda wa miezi saba.