Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 76:9 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Mungu aliposimama ili kuhukumu Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

wakati ulipoinuka kutekeleza hukumu, kuwaokoa wote wanaodhulumiwa duniani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

wakati ulipoinuka kutekeleza hukumu, kuwaokoa wote wanaodhulumiwa duniani.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

wakati ulipoinuka kutekeleza hukumu, kuwaokoa wote wanaodhulumiwa duniani.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Mungu aliposimama ili kuhukumu Na kuwaokoa wapole wa dunia wote pia.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 76:9
12 Marejeleo ya Msalaba  

Kwa kuwa BWANA awaridhia watu wake, Huwapamba wenye upole kwa wokovu.


Wenye upole atawaongoza katika haki, Wenye upole atawafundisha njia yake.


Na atawatetea watu walioonewa, Awaokoe wahitaji, na kumwaangamiza mdhalimu.


bali kwa haki atawahukumu maskini, naye atawaonya wanyenyekevu wa dunia kwa adili; naye ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake, na kwa pumzi ya midomo yake atawaua wabaya.


Wamenenepa sana, wang'aa; naam, wamepita kiasi kwa matendo maovu; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.


Lakini BWANA yumo ndani ya hekalu lake takatifu; dunia yote na inyamaze kimya mbele zake.


Mtafuteni BWANA, enyi nyote mlio wanyenyekevu wa dunia, ninyi mliozitenda hukumu zake; itafuteni haki, utafuteni unyenyekevu; huenda mtafichwa katika siku ya hasira ya BWANA.


BWANA akanena ghafla na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.


Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.


bali kuwe utu wa moyoni usioonekana, katika mapambo yasiyoharibika; yaani, roho ya upole na utulivu, iliyo ya thamani kuu mbele za Mungu.