Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mnyonge; akawatia wote mkononi mwake.
Zaburi 74:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako; Wameweka bendera zao ziwe alama. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Maadui zako wamenguruma ushindi hekaluni mwako! Wameweka humo bendera zao za ushindi! Biblia Habari Njema - BHND Maadui zako wamenguruma ushindi hekaluni mwako! Wameweka humo bendera zao za ushindi! Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Maadui zako wamenguruma ushindi hekaluni mwako! Wameweka humo bendera zao za ushindi! Neno: Bibilia Takatifu Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama. Neno: Maandiko Matakatifu Adui zako wamenguruma pale ulipokutana nasi, wanaweka bendera zao kama alama. BIBLIA KISWAHILI Watesi wako wamenguruma kati ya kusanyiko lako; Wameweka bendera zao ziwe alama. |
Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mnyonge; akawatia wote mkononi mwake.
Bwana ameitupilia mbali madhabahu yake, Amepachukia patakatifu pake; Amezitia katika mikono ya hao adui Kuta za majumba yake; Wamepiga kelele ndani ya nyumba ya BWANA Kama katika sikukuu.
Yeye huponya na kuokoa, hutenda ishara na maajabu mbinguni na duniani, ndiye aliyemponya Danieli na nguvu za simba.
Wana wa Israeli watapanga kila mtu penye bendera yake mwenyewe, na alama za nyumba za baba zao; kuikabili hema ya kukutania ndiko watakakopanga kwa kuizunguka pande zote.
Basi hapo mtakapoliona chukizo la uharibifu, lile lililonenwa na nabii Danieli, limesimama katika patakatifu (asomaye na afahamu),
Na wakati uo huo walikuwapo watu waliompasha habari ya Wagalilaya wale ambao Pilato alichanganya damu yao na dhabihu zao.
Lakini, hapo mtakapoona mji wa Yerusalemu umezungukwa na majeshi, basi jueni ya kwamba uharibifu wake umekaribia.
Akafunua kinywa chake amtukane Mungu, na kulitukana jina lake, na maskani yake, nao wakaao mbinguni.