Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 74:18 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ee BWANA, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Kumbuka, ee Mwenyezi-Mungu, madharau ya maadui zako; taifa pumbavu linalikashifu jina lako. Sisi ni dhaifu kama njiwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Kumbuka, ee Mwenyezi-Mungu, madharau ya maadui zako; taifa pumbavu linalikashifu jina lako. Sisi ni dhaifu kama njiwa.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Kumbuka, ee Mwenyezi-Mungu, madharau ya maadui zako; taifa pumbavu linalikashifu jina lako. Sisi ni dhaifu kama njiwa.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ee Mwenyezi Mungu, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki, jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ee bwana, kumbuka jinsi mtesi alivyokudhihaki, jinsi watu wapumbavu walivyolitukana jina lako.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ee BWANA, uyakumbuke hayo, adui amelaumu, Na watu wapumbavu wamelidharau jina lako.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 74:18
16 Marejeleo ya Msalaba  

Yamkini BWANA, Mungu wako, atayasikia maneno yote ya kamanda huyu, ambaye mfalme wa Ashuru, bwana wake, amemtuma ili amtukane Mungu aliye hai; naye atayakemea hayo maneno aliyoyasikia BWANA, Mungu wako; kwa sababu hii inua dua yako kwa ajili ya mabaki yaliyobakia.


Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu, kana kwamba kuitaja miungu ya mataifa wa nchi, iliyo kazi ya mikono ya watu.


Ee BWANA, uwakumbuke wana wa Edomu, Siku ile Yerusalemu ilipotekwa. Kwa namna walivyosema, Bomoeni! Bomoeni hata misingini!


Uniokoe kutoka kwa maasi yangu yote, Usinifanye niwe wa kulaumiwa na mpumbavu.


Heri amkumbukaye mnyonge; BWANA atamwokoa siku ya taabu.


Ee Mungu, usimame, ujitetee mwenyewe, Ukumbuke unavyotukanwa na mpumbavu mchana kutwa.


Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata; Utazame na kuiona aibu yetu.


Lakini nilitenda kwa ajili ya jina langu, lisitiwe unajisi machoni pa mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao.


Nanyi mmejitukuza juu yangu kwa vinywa vyenu, na kuyaongeza maneno juu yangu; nimesikia mimi.


Isipokuwa niliogopa makamio ya adui, Adui zao wasije wakafikiri uongo, Wasije wakasema, Mkono wetu umetukuka, Wala BWANA hakuyafanya haya yote.


Je! Mnamlipa BWANA hivi, Enyi watu wapumbavu na ujinga? Je! Yeye siye baba yako aliyekununua? Amekufanya, na kukuweka imara.


Na mji ule mkuu ukagawanyika katika mafungu matatu, na miji ya mataifa ikaanguka; na Babeli ule mkuu ukakumbukwa mbele za Mungu, kupewa kikombe cha mvinyo ya ghadhabu ya hasira yake.