Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 73:25 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mbinguni, nani awezaye kunisaidia ila wewe? Na duniani hamna ninachotamani ila wewe!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mbinguni, nani awezaye kunisaidia ila wewe? Na duniani hamna ninachotamani ila wewe!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mbinguni, nani awezaye kunisaidia ila wewe? Na duniani hamna ninachotamani ila wewe!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ni nani niliye naye mbinguni, Wala duniani sina cha kupendeza ila Wewe.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 73:25
19 Marejeleo ya Msalaba  

Kutafakari kwangu na kuwe kutamu kwake; Maana furaha yangu hutoka kwa BWANA.


Utanijulisha njia ya uzima; Mbele za uso wako kuna furaha tele; Na katika mkono wako wa kulia Mna mema ya milele.


Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu; Sina wema ila utokao kwako.


BWANA ndiye fungu la posho langu, Na la kikombe changu; Wewe unayaamua maisha yangu.


Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, Niamkapo nishibishwe kwa sura yako.


Nawe ujifurahishe katika BWANA, Naye atakutimizia haja za moyo wako.


Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu; Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.


Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai; Midomo yangu itakusifu.


Maana ni nani katika mbingu awezaye kulinganishwa na BWANA? Ni nani afananaye na BWANA miongoni mwa malaika?


Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili.


Heri wenye moyo safi; Maana hao watamwona Mungu.


Naam, zaidi ya hayo, nayahesabu mambo yote kuwa hasara kwa ajili ya uzuri usio na kiasi wa kumjua Kristo Yesu, Bwana wangu; ambaye kwa ajili yake nimepata hasara ya mambo yote nikiyahesabu kuwa kama mavi ili nipate Kristo;


Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini tunajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana naye; kwa maana tutamwona kama alivyo.


Nikasikia sauti kubwa kutoka katika kile kiti cha enzi ikisema, Tazama, maskani ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atafanya maskani yake pamoja nao, nao watakuwa watu wake. Naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.