Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 73:12 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe sikuzote wamepata mali nyingi.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Hivi ndivyo watu waovu walivyo; wana kila kitu na wanapata mali zaidi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Hivi ndivyo watu waovu walivyo; wana kila kitu na wanapata mali zaidi.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Hivi ndivyo watu waovu walivyo; wana kila kitu na wanapata mali zaidi.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Fahamu, ndivyo walivyo wasio haki, Na kwa kustarehe siku zote wamepata mali nyingi.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 73:12
11 Marejeleo ya Msalaba  

Ee BWANA, kwa mkono wako uniokoe na watu, Watu wa dunia hii ambao fungu lao liko katika maisha haya. Matumbo yao wayajaza kwa hazina yako, Hushiba wana, huwaachia watoto wao akiba zao,


Nimemwona mtu asiye haki mkali sana, Akijieneza kama mwerezi wa Lebanoni.


Ambao wanazitumainia mali zao, Na kujisifia wingi wa utajiri wao;


Kumbe! Huyu ndiye mtu yule, Asiyemfanya Mungu kuwa kimbilio lake. Aliutumainia wingi wa mali zake, Na kufanya mali kimbilio lake.


Msiitumainie dhuluma, Wala msijivune kwa unyang'anyi; Mali izidipo msiiangalie sana moyoni.


Nao watakula mavuno yako, na mkate wako, ambao iliwapasa wana wako na binti zako kuula; watakula makundi yako ya kondoo na ya ng'ombe; watakula mizabibu yako na mitini yako; wataiharibu miji yako yenye boma, uliyokuwa ukiitumainia, naam, wataiharibu kwa upanga.


Wamenenepa sana, wang'aa; naam, wamepita kiasi kwa matendo maovu; hawatetei madai ya yatima, ili wapate kufanikiwa; wala hawaamui haki ya mhitaji.


Akasema, Palikuwa na mtu mmoja, tajiri, aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, na kula sikuzote kwa anasa.