Mungu wa Israeli alisema, Mwamba wa Israeli aliniambia, Atawalaye wanadamu kwa haki, Akitawala katika kicho cha Mungu,
Zaburi 72:1 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, Na mwana wa mfalme haki yako. Matoleo zaidiBiblia Habari Njema Ee Mungu, umjalie mfalme uamuzi wako, umpe mwanamfalme uadilifu wako; Biblia Habari Njema - BHND Ee Mungu, umjalie mfalme uamuzi wako, umpe mwanamfalme uadilifu wako; Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza Ee Mungu, umjalie mfalme uamuzi wako, umpe mwanamfalme uadilifu wako; Neno: Bibilia Takatifu Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako. Neno: Maandiko Matakatifu Ee Mungu, mjalie mfalme aamue kwa haki yako, mwana wa mfalme kwa haki yako. BIBLIA KISWAHILI Ee Mungu, mpe mfalme hukumu zako, Na mwana wa mfalme haki yako. |
Mungu wa Israeli alisema, Mwamba wa Israeli aliniambia, Atawalaye wanadamu kwa haki, Akitawala katika kicho cha Mungu,
Na Sadoki, kuhani, akatwaa ile pembe ya mafuta katika Hema, akamtia Sulemani mafuta. Nao wakapiga panda; na watu wote wakasema, Na aishi Mfalme Sulemani!
Kwa hiyo nipe mimi mtumwa wako moyo wa adili niwahukumu watu wako, na kupambanua mema na mabaya; maana ni nani awezaye kuwahukumu watu hawa wako walio wengi?
tazama, utapata mwana, atakayekuwa mtu wa amani; nami nitampa amani mbele ya adui zake pande zote; kwani jina lake litakuwa Sulemani, nami nitawapa Israeli amani na utulivu siku zake;
naye Sulemani mwanangu, umjalie ili kwa moyo wote, azishike amri zako, na shuhuda zako, na maagizo yako, akayatende hayo yote na kuijenga nyumba hii ya enzi, niliyoiwekea akiba.
Basi sasa nipe hekima na maarifa, nijue kutoka na kuingia mbele ya watu hawa; kwa kuwa ni nani awezaye kuwatawala watu wako hawa walio wengi?
BWANA asipoijenga nyumba Waijengao wanafanya kazi bure. BWANA asipoulinda mji Yeye aulindaye anakesha bure.
Na Roho ya BWANA itakaa juu yake, roho ya hekima na ufahamu, roho ya shauri na uweza, roho ya maarifa na ya kumcha BWANA;
Kwa kuwa yeye aliyetumwa na Mungu huyanena maneno ya Mungu; kwa sababu hamtoi Roho kwa kipimo.