Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 7:4 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema, au nimemshambulia adui yangu bila sababu,

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema, au nimemshambulia adui yangu bila sababu,

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

kama nimemlipa rafiki yangu mabaya badala ya mema, au nimemshambulia adui yangu bila sababu,

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyang’anya adui yangu pasipo sababu,

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

au ikiwa nimemtenda uovu aliye na amani nami, au nimemnyang’anya adui yangu pasipo sababu,

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ikiwa nimemlipa mabaya Yeye aliyekaa kwangu salama; (Hasha! Nimemponya yeye Aliyekuwa mtesi wangu bila sababu;)

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 7:4
20 Marejeleo ya Msalaba  

Na walipotoka mjini, kabla hawajaendelea sana, Yusufu akamwambia yule msimamizi wa nyumba yake, Ondoka, uwafuate watu hawa, nawe utakapowapata, waambie, Kwa nini mmelipa mabaya kwa mema?


Atakayeonekana kuwa nacho miongoni mwa watumwa wako, na afe, na sisi nasi tutakuwa watumwa wa bwana wangu.


BWANA amerudisha juu yako damu yote ya nyumba ya Sauli ambaye umetawala badala yake; naye BWANA ametia ufalme katika mkono wa Absalomu mwanao; kisha, angalia, wewe umetwaliwa katika uovu wako mwenyewe, kwa sababu umekuwa mtu wa damu.


Basi bega langu na lianguke kutoka mahali pake, Na mkono wangu uvunjike mfupani mwake.


Kwamba hatua yangu imekengeuka na kuiacha njia, Na moyo wangu kuyaandama macho yangu, Tena kwamba kipaku chochote kimeshikamana na mikono yangu;


Wamenilipa mabaya kwa mema yangu, Na chuki badala ya upendo wangu.


Mwenzangu amenyosha mkono awadhuru waliopatana naye, Amelivunja agano lake.


Kalibu ni kwa fedha, na tanuri kwa dhahabu; Bali BWANA huijaribu mioyo.


Ila Paulo akapaza sauti yake kwa nguvu, akisema, Usijidhuru, kwa maana sisi sote tuko hapa.


Kisha Daudi akatoka Nayothi huko Rama, akakimbia, akaenda kwa Yonathani, akasema mbele yake, Nimefanya nini? Uovu wangu ni nini? Dhambi yangu mbele ya baba yako ni nini, hata akaitaka roho yangu?


Basi Ahimeleki akamjibu mfalme, akasema, Katika watumishi wako wote ni nani aliye mwaminifu kama Daudi, aliye mkwewe mfalme, tena msiri wako, mwenye heshima nyumbani mwako?


Basi Daudi akawazuia watu wake kwa maneno hayo, asiwaruhusu kumshambulia Sauli. Kisha Sauli akatoka pangoni, akaenda zake.


Ndipo Sauli akasema, Nimekosa; rudi, Daudi, mwanangu; maana sitakudhuru tena, kwa kuwa maisha yangu yalikuwa na thamani machoni pako leo; angalia, nimetenda upumbavu, nimekosa sana.


Tena, angalia, kama vile maisha yako yalivyokuwa na thamani machoni pangu, kadhalika na maisha yangu na yawe na thamani machoni pa BWANA, akaniokoe katika shida zote.