Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 7:10 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Mungu ndiye ngao yangu; yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Mungu ndiye ngao yangu; yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Mungu ndiye ngao yangu; yeye huwaokoa wanyofu wa moyo.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Ngao yangu ni Mungu Aliye Juu Sana, anayewaokoa wanyofu wa moyo.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Ngao langu ni Mungu Aliye Juu Sana, awaokoaye wanyofu wa moyo.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Ngao yangu ina Mungu, Awaokoaye wanyofu wa moyo.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 7:10
15 Marejeleo ya Msalaba  

Baada ya mambo hayo neno la BWANA likamjia Abramu katika njozi, likinena, Usiogope, Abramu, Mimi ni ngao yako, na thawabu yako itakuwa kubwa sana.


Nawe, Sulemani mwanangu, mjue Mungu wa baba yako, ukamtumikie kwa moyo mkamilifu, na kwa nia ya kumkubali; kwa kuwa BWANA huchunguza mioyo yote, na kuyatambua mawazo yote ya fikira; ukimtafuta, atakuwa nawe; ukimwacha, atakutupa milele.


basi usikie huko mbinguni, ukaapo, ukasamehe, ukampatilize kila mtu kwa kadiri ya njia zake zote; wewe umjuaye moyo; (maana wewe peke yako ndiwe uijuaye mioyo ya wanadamu);


Ikiwa wewe u safi na mwelekevu; Hakika yeye sasa angeamka kwa ajili yako, Na kuyafanya makazi ya haki yako kufanikiwa.


Wazawa wake watakuwa hodari duniani; Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.


Ee BWANA, uwatendee mema walio wema, Nao walio wanyofu wa moyo.


Lakini Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote, Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.


Kwa kuwa BWANA, Mungu, ni jua na ngao, BWANA atatoa neema na utukufu. Hatawanyima kitu chema Hao waendao kwa ukamilifu.


Maana ngao yetu ni BWANA, Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli.


Wenye uhalifu moyoni ni chukizo kwa BWANA; Walio wakamilifu katika njia zao humpendeza.


Maana wanyofu watakaa katika nchi, Na wakamilifu watadumu ndani yake.


Aendaye kwa unyofu ataokolewa; Bali mkaidi wa njia zake ataanguka mara.


Lakini, Ee BWANA wa majeshi, uhukumuye haki, ujaribuye fikira na moyo, nijalie kuona kisasi chako juu yao; kwa maana nimekufunulia wewe neno langu.


Mimi, BWANA, nauchunguza moyo, navijaribu viuno, hata kumpa kila mtu kiasi cha njia zake, kiasi cha matunda ya matendo yake.