Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 69:3 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo yangu imekauka. Macho yangu yamedhoofika Kwa kumngoja Mungu wangu.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Niko hoi kwa kupiga yowe, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Niko hoi kwa kupiga yowe, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Niko hoi kwa kupiga yowe, na koo langu limekauka. Macho yangu yamefifia, nikikungojea ewe Mungu wangu.

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Nimechoka kwa kuomba msaada, koo langu limekauka. Macho yangu yanafifia, nikimtafuta Mungu wangu.

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Nimechoka kwa kulia kwangu, Koo langu limekauka. Macho yangu yamedhoofika Kwa kumngoja Mungu wangu.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 69:3
18 Marejeleo ya Msalaba  

Lakini macho ya waovu yataingia kiwi, Nao hawatakuwa na njia ya kukimbilia, Na matumaini yao yatakuwa ni kutoa roho.


Uso wangu umeharibika kwa kutoa machozi, Na giza tupu liko katika kope zangu;


Macho yangu yanafifia kwa kuungojea wokovu wako, Na kutimizwa kwa ahadi yako ya haki.


Macho yangu yamefifia kwa kuitazamia ahadi yako, Nikisema, Lini utakaponifariji?


Nguvu zangu zimekauka kama gae, Ulimi wangu waambatana na taya zangu; Unaniweka katika mavumbi ya mauti


Ee Mungu wangu, nalia mchana lakini hujibu Na wakati wa usiku lakini sipati raha.


Ukamilifu na unyofu zinihifadhi, Maana nakungoja Wewe.


Na sasa ninangoja nini, Ee Bwana? Matumaini yangu ni kwako.


Akatia wimbo mpya kinywani mwangu, Ndio sifa zake Mungu wetu. Wengi wataona na kuogopa, Nao watamtumainia BWANA.


Nimechoka kwa kuugua kwangu; Kila usiku nakibubujikia kitanda changu; Nililowesha godoro langu kwa machozi yangu.


Wakanipa uchungu kuwa chakula changu; Na nilipokuwa na kiu wakaninywesha siki.


Ghadhabu yako imenilemea, Umenitesa kwa mawimbi yako yote.


Kama mbayuwayu au korongo ndivyo nilivyolia; Niliomboleza kama hua; macho yangu yamedhoofu kwa kutazama juu; Ee BWANA, nimeonewa, na uwe mdhamini wangu.


Macho yangu yamechoka kwa machozi, Mtima wangu umetaabika; Ini langu linamiminwa juu ya nchi Kwa uharibifu wa binti ya watu wangu; Kwa sababu watoto wachanga na wanyonyao, Huzimia katika mitaa ya mji.


Baada ya hayo Yesu, hali akijua ya kuwa yote yamekwisha kumalizika ili andiko litimizwe, akasema, Naona kiu.


Wanao na binti zako litapewa taifa lingine, na macho yako yataangalia, na kuzimia kwa kuwatamani mchana kutwa; wala hapatakuwa na kitu katika uwezo wa mkono wako.


Yeye, siku hizo za mwili wake, alimtolea yule, awezaye kumwokoa na kumtoa katika mauti, maombi na dua pamoja na kulia sana na machozi, akasikilizwa kwa jinsi alivyokuwa mcha Mungu;