Biblia ya mtandaoni

Matangazo


Biblia nzima Agano la Kale Agano Jipya




Zaburi 66:2 - Swahili Revised Union Version - SRUVDC

Imbeni utukufu wa jina lake, Tukuzeni sifa zake.

Tazama sura

Matoleo zaidi

Biblia Habari Njema

Imbeni juu ya utukufu wa jina lake, mtoleeni sifa tukufu!

Tazama sura

Biblia Habari Njema - BHND

Imbeni juu ya utukufu wa jina lake, mtoleeni sifa tukufu!

Tazama sura

Biblia Habari Njema: Toleo la Kujifunza

Imbeni juu ya utukufu wa jina lake, mtoleeni sifa tukufu!

Tazama sura

Neno: Bibilia Takatifu

Imbeni utukufu wa jina lake; mpeni sifa zake kwa utukufu!

Tazama sura

Neno: Maandiko Matakatifu

Imbeni utukufu wa jina lake; mpeni sifa zake kwa utukufu!

Tazama sura

BIBLIA KISWAHILI

Imbeni utukufu wa jina lake, Tukuzeni sifa zake.

Tazama sura
Tafsiri zingine



Zaburi 66:2
17 Marejeleo ya Msalaba  

Ndipo Walawi, Yeshua na Kadmieli, na Bani, na Hashabneya, na Sherebia, na Hodia, na Shebania, na Pethahia, wakasema, Simameni, mkamhimidi BWANA, Mungu wenu, tangu milele na hata milele. Na lihimidiwe jina lako tukufu, lililotukuka kuliko baraka zote na sifa zote.


Nani awezaye kuyanena matendo makuu ya BWANA, Au kuzihubiri sifa zake zote?


Na wamshukuru BWANA kwa fadhili zake, Na maajabu yake kwa wanadamu.


Na wamtolee dhabihu za kushukuru, Na kuyasimulia matendo yake kwa kuimba.


Apandaye mbingu za mbingu za tangu milele; Aitoa sauti yake, sauti ya nguvu.


Na ahimidiwe BWANA, Mungu, Mungu wa Israeli, Atendaye miujiza Yeye peke yake;


Ee Mungu wa wokovu wetu, utusaidie, Kwa ajili ya utukufu wa jina lako. Utuokoe, utusamehe dhambi zetu, Kwa ajili ya jina lako.


Na wamtukuze BWANA, Na kutangaza sifa zake visiwani.


Imbeni, enyi mbingu; ufurahi, Ee nchi; Pazeni sauti ya kuimba, enyi milima; Kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake, Naye atawahurumia watu wake walioteswa.


Wakaitana, kila mmoja na mwenzake, wakisema, Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.


Na kila kiumbe kilichoko mbinguni na juu ya nchi na chini ya nchi na juu ya bahari, na vitu vyote vilivyomo ndani yake, nilivisikia, vikisema, Baraka na heshima na utukufu na uweza una yeye aketiye juu ya kiti cha enzi, na kwake Mwana-kondoo, hata milele na milele.